Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Vijana Huuliza . . . Je, Nina Tatizo la Kula? (Oktoba 2006) Baada ya kusoma makala hiyo, nilishuka moyo. Nimekabiliana na tatizo la kula katika maisha yangu yote. Makala hiyo ilinifanya nihisi kwamba nilipaswa “kutatua” tatizo hilo nilipokuwa mdogo. Lakini, mpaka leo ninakabiliana na jinamizi hilo na sasa ninahisi sina tumaini. Kulingana na makala hiyo ilionekana kana kwamba mtu anaweza kushinda tatizo hilo ikiwa tu ana imani thabiti.

J. J., Marekani

“Amkeni!” lajibu: Ingawa makala zinazozungumziwa kwenye “Vijana Huuliza . . . ” zinakazia fikira hasa vijana, kanuni za Biblia zilizo kwenye makala hizo zinahusu watu wa rika lolote. Tunatambua kwamba matatizo ya kula ni baadhi ya magonjwa magumu zaidi kuponya. Makala haikusema wanaokabiliana na matatizo ya kula hawana imani. Ilidokeza tu kwamba wenye matatizo hayo wanaweza kusali kwa Yehova awasaidie kukabiliana na matatizo ya kula. Zaidi ya kumsihi Mungu, walio na tatizo wanaweza kutafuta msaada kutoka kwa “mzazi au mtu mzima mwingine.” Pia makala ilieleza “si rahisi kushinda tatizo hilo” na kwamba kuna uwezekano wa kulirudia. Na pia kwa sababu umesema bado unajaribu kukabiliana na tatizo la kula inamaanisha hujakata tamaa.

Vijana Huuliza . . . Niyatumieje Maisha Yangu? (Julai 2006) Karibuni nitamaliza masomo yangu, na nimefikia wakati ninapaswa kupanga jinsi nitakavyoyatumia maisha yangu. Makala hii imenisaidia kuazimia hata zaidi kufuata mradi wa kuingia katika utumishi wa wakati wote. Hakuna kazi nyingine inayofaa au itakayoniletea shangwe zaidi kuliko hiyo.

H. W., Hong Kong

Nimefurahi sana kupata makala hii kwa sababu imenisaidia kuona kwamba katika ulimwengu huu unaofuatia mambo ya kimwili, jambo bora zaidi kwa kijana kama mimi ni kutanguliza miradi ya kiroho.

A. S., Brazili

Katika maisha yangu yaliyojaa shughuli, mimi hushindwa kukazia fikira miradi yangu. Lakini kusoma makala hii kumenisaidia kuazimia upya kufanya yote niwezayo kumtumikia Yehova. Asanteni sana kwa kutujali sisi vijana.

E. M., Japani

Jinsi ya Kuwa na Ndoa Yenye Furaha (Julai 2006) Makala hizi zimeandikwa kwa ustadi wa hali ya juu. Mfano ambao Yesu aliwawekea wenzi wa ndoa kwa kuwatendea vema wanafunzi wake ulifaa sana. Endeleeni na kazi yenu nzuri. Tunangojea kwa hamu magazeti ya kila mwezi.

S. C., Marekani

Sikuwa na Tumaini Lakini Sasa Nina Furaha (Julai 2006) Kama Ndugu González, mimi pia hujiona sifai. Nilifikiri, ‘Yehova hawezi kumpenda mtenda dhambi kama mimi.’ Ni baraka iliyoje kujua jinsi Yehova anavyosamehe, na jinsi alivyo na upendo na rehema! Kupitia mashauri, kutegemezwa kwa upendo na kutaniko, na roho takatifu ya Yehova, nimepata msaada wa kutumia kweli za Biblia maishani mwangu. Asante kwa chakula hiki cha kiroho cha wakati unaofaa.

T. A., Marekani