Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Ndicho Kitabu Tulichohitaji Hasa!”

“Ndicho Kitabu Tulichohitaji Hasa!”

“Ndicho Kitabu Tulichohitaji Hasa!”

Hivyo ndivyo mama mmoja huko Italia alivyosema alipopata kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. “Nisingejizuia kulia,” anasema. Anasema hivi pia kuhusu binti yake mchanga: “Ingawa bado hawezi kusoma, anakumbuka mambo makuu kwa sababu ya picha. Yeye husikiliza kwa makini kwa sababu kitabu kimeandikwa kana kwamba ni mazungumzo pamoja na msomaji, naye hushiriki mazungumzo hayo mara nyingi. Hii ni zawadi bora zaidi ambayo mtu yeyote angewahi kutupa.”

Baba mmoja huko Italia anaeleza kwamba yeye na mke wake wamekuwa wakijiuliza jinsi watakavyomweleza mtoto wao mambo yanayohusu ngono. Wazazi hao wanasema: “Kitabu hicho kipya kilipotolewa, tulihisi kwamba Mungu ametambua mahangaiko yetu. Baada ya kukichunguza, tuliona jinsi kitabu hicho kipya kinavyomsaidia mwana wetu kufikiri na kutafakari.”

Kijana mmoja huko Japani aliyetendewa vibaya kingono akiwa mtoto, aliandika hivi kwa uthamini: “Nililia sana na kumshukuru Yehova mara nyingi sana. Kitabu hicho kinaeleza waziwazi na kwa usahihi mambo ambayo watoto wanaweza kukabiliana nayo katika nyakati hizi za uovu. Maswali yaliyomo yanaufikia moyo wa mtoto mdogo. Sura ya 32 ni yenye thamani kama nini katika kulinda watoto dhidi ya watu wazima waovu! Maisha yangu yangekuwa tofauti sana ikiwa ningepata kitabu hicho chenye kuelimisha na kinachoeleza mambo waziwazi miaka 20 iliyopita.”

Unaweza kuomba kitabu hicho kilicho na kurasa zinazolingana na gazeti hili, chenye kurasa 256 na picha za kupendeza. Jaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Bila masharti ningependa kupokea kitabu kilichoonyeshwa hapa.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.