Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mafundisho ya Kimungu Huwa na Matokeo Mazuri

Mafundisho ya Kimungu Huwa na Matokeo Mazuri

Mafundisho ya Kimungu Huwa na Matokeo Mazuri

Mara nyingi wazazi ambao huwafundisha watoto wao tangu wakiwa wachanga hupata matokeo mazuri kutokana na jitihada zao. Dorian, kijana kutoka Peru, Amerika Kusini, alitoa hotuba yake ya kwanza katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova alipokuwa na umri wa miaka minne. Alipoanza kwenda shule, angeweza kutumia Biblia kumweleza mwalimu na wanafunzi wenzake kwa nini yeye hasherehekei Krismasi.

Hivi karibuni, alipokuwa na umri wa miaka mitano, Dorian aliombwa atoe hotuba mbele ya shule nzima, yaani, mbele ya wanafunzi 500 hivi na kueleza maoni yake kuhusu Sikukuu ya Akina Baba. Alitayarisha hotuba ya dakika kumi yenye kichwa “Madaraka ya Baba,” ikitegemea Waefeso 6:4. Mwisho wa hotuba yake alisema, “Badala ya kusherehekea Sikukuu ya Akina Baba siku moja kwa mwaka, watoto wanapaswa kuwaheshimu na kuwatii wazazi wao kila siku.”

Mnamo 1943, Mashahidi wa Yehova walianzisha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, ambayo ilikusudiwa kuwasaidia wote, wakubwa kwa wadogo, wawe wasemaji wazuri mbele za watu. Shule hiyo inafanywa kila juma. Tangu wakati huo, imewapa watoto mafunzo yanayotegemea Biblia kuongezea mafundisho ambayo wazazi wao wanapaswa kuwapa.—Methali 22:6.

Mnamo Novemba 2005, Simon, kijana anayeishi Uswisi alitoa hotuba yake ya kwanza katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi akiwa na umri wa miaka sita. Mwaka mmoja hivi baadaye, alihojiwa kwenye programu ya kusanyiko kubwa la Mashahidi wa Yehova. Alikuwa amesitawisha mtazamo gani kuelekea mambo ya kiroho?

Simon hupenda kuhudhuria mikutano ya Kikristo na hakosi mkutano wowote hata akiwa amechoka. Isitoshe, yeye huenda shambani pamoja na wengine katika familia. Kila mwezi, yeye huwaachia watu wa umri wote magazeti kati ya 30 hadi 50 ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Zaidi ya hayo, mara nyingi yeye huzungumza na baba yake kuhusu Biblia na kumtia moyo aandamane na wengine katika familia wanapohudhuria mikutano.

Bila shaka, wazazi ambao huwalea watoto wao “katika nidhamu na mwongozo wa akilini wa Yehova,” wanapata shangwe nyingi watoto wao wanapotii na kuzaa tunda la uadilifu.—Waefeso 6:4; Yakobo 3:17, 18.

[Picha katika ukurasa wa 28]

Dorian akiwa shuleni

[Picha katika ukurasa wa 28]

Simon akiwa kwenye Jumba la Ufalme