Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Tafuta Mashauri Mazuri

Tafuta Mashauri Mazuri

Hatua ya 1

Tafuta Mashauri Mazuri

Kwa nini hatua hii ni muhimu? Mara ya kwanza wazazi wanapombeba mtoto wao mchanga, huenda wakawa na hisia mbalimbali. “Nilikuwa na shangwe na niliduwaa,” anasema Brett, baba anayeishi Uingereza. “Lakini pia nilihisi kuwa nina jukumu kubwa sana ambalo sikuona ikiwa ninaweza kulitimiza.” Monica, mama anayeishi Argentina, anasema: “Nilikuwa na wasiwasi kwamba sitaweza kumtimizia binti yangu mahitaji yake. Nilijiuliza, ‘Je, nitaweza kumlea afikie kuwa mtu mzima mwenye kutegemeka?’”

Je, unaweza kuelewa shangwe na wasiwasi wa wazazi hao? Kwa kweli, kati ya kazi ambazo mtu anaweza kufanya, kumlea mtoto ni kazi inayochosha na kutamausha lakini inayoridhisha na kuthawabisha. Baba mmoja alisema, “mtu huwa mtoto mara moja tu maishani hivyo una nafasi moja tu ya kumlea.” Kwa kuwa sehemu kubwa ya afya na furaha ya watoto hutegemea hasa uvutano wa wazazi, huenda ukataka sana kupata mashauri yanayotegemeka ya jinsi unavyoweza kuwa mzazi bora.

Tatizo: Inaonekana kwamba kila mtu ana mashauri ya jinsi ya kulea watoto. Zamani wazazi walipopata mtoto wao wa kwanza walifuata hasa mfano wa wazazi wao au mafundisho yao ya kidini. Lakini katika nchi kadhaa, familia zinazorota na dini haziwavutii tena watu. Kwa sababu hiyo, wazazi wengi hutafuta mashauri kutoka kwa wataalamu wa kulea watoto. Mambo fulani ambayo wataalamu hao husema yanategemea kanuni zinazofaa. Kwa upande mwingine, mashauri ya wataalamu kama hao yanaweza kupingana na baada ya muda yanaweza kuonwa kuwa yamepitwa na wakati.

Suluhisho: Tafuta mashauri ya Yule anayejua vizuri zaidi jinsi ya kuwalea watoto—Muumba wa wanadamu, Yehova Mungu. (Matendo 17:26-28) Neno lake, Biblia, lina mashauri ya moja kwa moja na mifano halisi ambayo inaweza kukusaidia kuwa mzazi bora. Anaahidi hivi, “Nitakupa shauri jicho langu likiwa linakutazama.”—Zaburi 32:8.

Mungu anawapa wazazi mashauri gani ambayo yanaweza kuwasaidia kulea watoto wenye furaha?

[Blabu katika ukurasa wa 3]

“Mtegemee Yehova kwa moyo wako wote wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe.”—Methali 3:5