Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kinapendwa Kuliko Vifaa vya Kuchezea

Kinapendwa Kuliko Vifaa vya Kuchezea

Kinapendwa Kuliko Vifaa vya Kuchezea

Je, watoto wadogo wanaweza kupenda kitabu kuliko vifaa vya kuchezea? Wanaweza iwapo tu wazazi wataanza kuwasomea vitabu wakiwa wadogo. Mebrahdtu na Angela ni wenzi wa ndoa huko California, Marekani, nao walianza kumsomea binti yao kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu tangu alipozaliwa.

Wazazi hao waliandika hivi: “Matokeo yamekuwa kwamba, anakipenda sana kitabu Mwalimu. Alipokuwa na umri wa miezi 12, alianza kutuomba tumsomee kile alichokiita kitabu cha Yesu. Sasa Julianna ana umri wa miaka mitatu, naye hutazamia sana vipindi anavyokuwa navyo pamoja na Mama au Baba kila siku. Hatutilii chumvi tukisema kwamba binti yetu anapenda kitabu hicho kuliko kifaa chochote cha kuchezea. Picha na mifano ya kitabu hicho, ni vifaa vyenye thamani vya kufundishia. Sisi tukiwa wazazi wake, tunajifunza mengi pia.”

Unaweza kuomba kitabu hicho chenye kurasa 256 na picha za kupendeza, kilicho na kurasa zenye ukubwa unaolingana na kurasa za gazeti hili. Jaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

❑ Bila masharti, ningependa kupokea kitabu kilichoonyeshwa hapa.

❑ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.