Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Ni Kizuri Sana!”

“Ni Kizuri Sana!”

“Ni Kizuri Sana!”

▪ HIVYO ndivyo msimamizi wa uchunguzi mmoja kuhusu ndoa alivyokifafanua kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Wenzi wa ndoa walioshiriki katika uchunguzi huo walimpa kitabu hicho na kumweleza kwamba kiliwasaidia kujitayarisha kwa ajili ya ndoa.

Msimamizi huyo aliandika barua ya kuwashukuru kwa “zawadi nzuri” waliyomtumia. Kisha alisema anatumaini kwamba wenzi wa ndoa kama hao wangewafundisha wengine “kinachohitajiwa ili ndoa iwe imara na yenye furaha.” Alikuwa na hakika kwamba vitabu kama Siri ya Kupata Furaha ya Familia, vingewasaidia wenzi hao washughulikie matatizo ambayo yangetokea. Msimamizi huyo alisema kwamba wenzi hao wana ndoa nzuri kwa kuwa wana imani thabiti na wanategemea msaada wa Mungu.

Msimamizi huyo alisema kwamba aliweka kitabu hicho juu ya dawati lake, naye huwaonyesha wanafunzi wake wanapomwomba mashauri kuhusu ndoa. Anamalizia kwa kusema hivi: “Sikuwa nimeona kitabu hicho hapo awali na ni kizuri sana!”

Kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia kimesaidia wenzi wengi wa ndoa duniani pote. Kinaweza pia kukusaidia kutumia kanuni za Biblia ambazo zitafanya maisha yako ya familia yawe yenye kufurahisha zaidi.

Unaweza kuomba kitabu hicho chenye kurasa 192 kwa kujaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Bila masharti, ningependa kupokea kitabu kilichoonyeshwa hapa.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.