Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Msaada Katika Kipindi cha Kuomboleza

Msaada Katika Kipindi cha Kuomboleza

Msaada Katika Kipindi cha Kuomboleza

▪ Mwanamke mmoja alipokuwa na umri wa miaka 12, baba yake alikufa. Kwa miaka mingi baada ya tukio hilo, alikabili mahangaiko na mshuko wa moyo. Alieleza hivi katika barua aliyoandikia ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova huko Kanada:

“Sikupata faraja mpaka niliposoma broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa na ilinisaidia sana katika kipindi hicho cha kuomboleza. Bado mimi hulia ninapofikiria jinsi ninavyomkosa sana baba yangu. Lakini baada ya kusoma, kutafakari, kusali, na kulia ninaposoma broshua hiyo na maandiko, sihisi huzuni sana kama zamani na sasa ninaweza kufarijiwa na ahadi za Mungu.

“Ninathamini sana maneno na maandiko yaliyo katika broshua hii kwa sababu yamesaidia sana kuuponya moyo wangu uliovunjika. Ninahisi mzima tena. Ninapendekeza broshua hii kama msaada katika kipindi cha kuomboleza.”

Je, kuna mtu yeyote unayempenda ambaye amelala katika usingizi wa kifo? Je, bado unaomboleza? Je, unahitaji msaada wa kukabiliana na huzuni yako? Biblia inatoa tumaini gani kwa watu waliokufa? Pengine wewe au mtu unayemfahamu atafarijiwa kwa kusoma broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa yenye kurasa 32. Unaweza kuomba broshua hiyo kwa kujaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Bila masharti, ningependa kupokea broshua iliyoonyeshwa hapa.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.