Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Ungejibuje?

Ungejibuje?

Ungejibuje?

Eleza Maana ya Mfano

1. Katika mfano uliorekodiwa kwenye Luka 18:9-14, Farisayo alikuwa mtu wa aina gani?

(Tia alama kwenye sanduku moja au zaidi hapa chini.)

□ Mnyenyekevu □ Mwenye kutubu □ Mwenye kiburi

2. Mkusanya-kodi alikuwa mtu wa aina gani?

(Tia alama kwenye sanduku moja au zaidi hapa chini.)

□ Mnyenyekevu □ Mwenye kutubu □ Mwenye kiburi

3. Kati ya watu hao wawili, ni yupi aliyethibitishwa kuwa mwadilifu zaidi?

․․․․․

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Ni nini kinachoweza kufanya uwe kama yule Farisayo kwa maneno au matendo? Unaweza kumwigaje mkusanya-kodi?

Katika Toleo Hili

Jibu maswali haya na utaje mistari ya Biblia ambayo haijaonyeshwa.

UKURASA WA 8-9 Wakati ujao wa dunia umo mikononi mwa nani? Isaya 11:________

UKURASA WA 20 Mungu ana maoni gani kuhusu sanamu za kidini? Kutoka 20:________

UKURASA WA 21 Mtume Yohana alionya kwamba tunapaswa kujilinda dhidi ya nini? 1 Yohana 5:________

UKURASA WA 27 Mara kwa mara, hata mtu mwadilifu sana atatambua nini? 1 Yohana 2:________

Watoto Watafute Picha

Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.

Ni Nani Aliye Katika Nasaba ya Yesu?

Fikiria madokezo. Soma maandiko. Kisha uandike majina sahihi katika nafasi zilizoonyeshwa.

4. ․․․․․

DOKEZO: Nilikuwa na uwezo wa kusema methali elfu tatu, na nyimbo zangu “zikawa elfu moja na tano.”

Soma 1 Wafalme 4:30-32.

5. ․․․․․

DOKEZO: Nilikuwa mfalme wa mwisho wa ufalme ulioungana wa Israeli.

Soma 1 Wafalme 12:1-3, 16-20.

6. ․․․․․

DOKEZO: Jeshi langu lilishinda jeshi kubwa la Yeroboamu kwa sababu ‘tulimtegemea Yehova.’

Soma 2 Mambo ya Nyakati 13:13-20.

▪ Majibu kwenye ukurasa wa 19

MAJIBU YA UKURASA WA 31

1. Mwenye kiburi.

2. Mnyenyekevu na mwenye kutubu.

3. Mkusanya-kodi.

4. Sulemani.—Mathayo 1:6.

5. Rehoboamu.—Mathayo 1:7.

6. Abiya.—Mathayo 1:7.