Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Hatua Saba za Kuwa Mzazi Bora (Agosti 2007) Gazeti hilo lilijibu sala zangu. Nina binti mwenye umri wa miaka minne anayempenda Yehova, lakini ninaogopa kwamba sitamlea vizuri. Hivyo, ninamwomba Yehova kila siku anisaidie kumzoeza. Asanteni sana kwa kutuhangaikia sisi wazazi.

Y.M.A., Mexico

Makala hizo zilikuwa kama kitabu cha mwongozo kilichoandikwa hasa kwa ajili ya familia yetu. Zilizungumzia masuala mengi yaliyokuwa yakinilemea akilini! Zilinithibitishia zaidi jinsi Yehova anavyowajali watu wake. Amesikiliza sala zangu na kuona machozi yangu na anajua jinsi nilivyohitaji habari hiyo.

J. M., Marekani

Katika kurasa chache tu, mlitia ndani mwongozo na mashauri muhimu yaliyo na matokeo bora. Sasa tunahitaji tu kufuata mwongozo huo!

E. L., Finland

Je, Kuwa na Mtazamo Mzuri Kunaweza Kuboresha Afya Yako? (Septemba 2007) Makala hii ilinisaidia sana, kwa kuwa mara nyingi nilijilaumu kwa matatizo niliyopata. Hivyo, nilifikiri kwamba sikuwa mama mzuri na nilifadhaika sana. Ingawa haikuwa rahisi kuwa na mtazamo mzuri, habari hiyo ilinisaidia kupunguza wasiwasi. Ninashukuru kwa jinsi mlivyotufikiria mlipoandika makala hiyo.

A. S., Ekuado

Historia ya Maumivu ya Meno (Septemba 2007) Mimi ni daktari wa meno na mwalimu wa matibabu ya meno. Nilipendezwa na jinsi mlivyoandika makala hiyo vizuri na kwa njia yenye kueleweka. Ilieleza vizuri historia ya matibabu ya meno. Nimewaonyesha makala hiyo marafiki wangu wengi na wafanyakazi wenzangu.

C. R., Marekani

Je, Mungu Anapaswa Kulaumiwa? (Septemba 2007) Mimi na rafiki zangu tulikutana ili kuzungumzia njia zinazofaa za kujitayarisha kwa ajili ya hali za dharura. Sisi hufurahia vinywaji, tunapitia madokezo katika sanduku “Je, Uko Tayari Kukimbia?” katika makala iliyotajwa hapo juu, na kuchunguza mifuko ya dharura ambayo baadhi yetu tumetayarisha. Pia sisi huzungumzia umuhimu wa kuwa na maoni yaliyosawazika kuhusu kujitayarisha kwa ajili ya dharura. Tunatambua kwamba kazi kuu tukiwa watumishi wa Mungu si kukusanya vitu tukijitayarishia misiba. Badala yake, ni kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu na kuwaambia watu juu ya ahadi nzuri ya Mungu kuhusu dunia ambayo haitakuwa na misiba yoyote ya asili au ile inayosababishwa na wanadamu.

R. G., Marekani

Walinde Watoto Wako! (Oktoba 2007) Nilitendewa vibaya kingono nilipokuwa mtoto. Bado siwezi kuwaambia wazazi wangu kilichonipata. Kwa hiyo, nilifarijiwa sana na makala hizo. Ninatumaini kwamba wazazi watasoma gazeti hilo na kuwalinda watoto wao. Ninamshukuru sana Yehova kwa kutupa habari hiyo muhimu ambayo imetufariji sana sisi tuliotendewa vibaya kingono.

R. I., Japani