Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Niliacha Kuwa Mtumwa wa Kileo (Mei 2007) Ninapoletewa magazeti yenu na Mashahidi mimi hufurahia kuyasoma. Inaburudisha kusoma makala zenu kuliko kupata habari zenye kuhuzunisha kwenye televisheni na katika magazeti. Sijawahi kuwa mraibu wa kileo, lakini nina washiriki wa familia na marafiki walio na uraibu huo. Mwanamume aliyetajwa katika makala hiyo alisema kwamba alishinda uraibu wake baada ya miezi mitatu. Na kwamba hiyo ilikuwa baada ya kuishi maisha yenye kuhuzunisha kwa sababu ya kileo. Ingawa ninampongeza, lazima niseme kwamba ni vigumu kuamini mfano wake, nami ninaona kwamba unaweza kumvunja moyo mtu yeyote anayekabiliana na tatizo hilo. Kwa kawaida, mraibu wa kileo huwa anarudia zoea hilo mara kadhaa anapojaribu kushinda tatizo hilo ngumu.

G. A., Marekani

“Amkeni!” lajibu: Hatukumaanisha kwamba ni rahisi kushinda uraibu wa kileo. Tunakubali kwamba watu wengi wanaokabiliana na uraibu wa kileo wanarudia zoea hilo na wanavunjika moyo kabla ya kulishinda. Hata wale ambao huacha kunywa kileo ghafula na wanaacha uraibu huo wanahitaji kuwa chonjo wasirudie zoea hilo tena. Hivyo, kama makala hiyo ilivyosema, baada ya miaka kumi kupita bila kunywa kileo, mtu huyo aliyekuwa “mtumwa wa kileo” alisema hivi: “Wengi hawajui jitihada kubwa ninayofanya na kwamba kunywa tu kiasi kidogo kunaweza kunifanya nirudie hali yangu ya zamani. Tamaa ya kunywa kileo ipo bado ndani yangu. Ninahitaji kusali sana na jitihada nyingi ili kukataa kileo.” Kwa kumtegemea Mungu katika sala, wengi wamefaulu kuacha kuwa watumwa wa kileo.—Zaburi 55:22.

Je, Unaweza Kuitegemea Biblia? (Novemba 2007) Nina umri wa miaka 12 na ningependa kuwashukuru kwa toleo hilo la pekee la Amkeni! linalopendeza na lenye habari nyingi. Nilifurahia hasa sehemu katika ukurasa wa 7 kuhusu upatano wa Biblia. Ilizungumzia mambo ambayo sikuwa nimewahi kuyafikiria mbeleni. Tayari ninangojea kwa hamu toleo la pekee linalofuata!

D. F., Marekani

Mambo ya Kufikiria Ningependa kuwashukuru kwa sababu ya mpangilio mpya wa Amkeni! Maswali yanayoulizwa mwishoni mwa makala mbalimbali yamenisaidia sana. Yamenisaidia kukumbuka habari hiyo na kufikiria kuihusu. Tunaishi katika kipindi chenye shughuli nyingi hivi kwamba tunaposoma tunaweza kukosa kutambua habari fulani muhimu na zenye kujenga.

M.A.S., Brazili

Je, Kweli Kifo Ndio Mwisho? (Desemba 2007) Miezi sita iliyopita, nilimpoteza mama yangu katika aksidenti mbaya. Nilitiwa moyo sana niliposoma makala hiyo kwani iliimarisha tumaini langu kwamba nitamwona tena wakati wa ufufuo. Asanteni sana.

L.L.R., Brazili

Vijana Huuliza . . . kwa Nini Niishi Kupatana na Viwango vya Biblia? (Novemba 2007) Nilidhani kwamba ikiwa singefanya uasherati, hakukuwa na ubaya kufanya urafiki wa karibu na mtu wa jinsia tofauti. Lakini sikuridhika tu kuwa pamoja na rafiki yangu wa jinsia tofauti. Nilianza kuwa na tamaa za kimwili zisizofaa. Asanteni sana kwa kueleza mafundisho hayo ya Biblia kwa njia ambayo ni rahisi kwa vijana wasio na uzoefu kuelewa.

E. F., Japani