Ungejibuje?
Ungejibuje?
Ilitukia Wapi?
1. Yesu alienda mbinguni kutoka mahali gani?
DOKEZO: Soma Matendo 1:6-12.
Chora mviringo kwenye jibu lako katika ramani.
Mlima Karmeli
Mlima Gerizimu
Mlima wa Mizeituni
Hebroni
▪ Kabla tu Yesu hajapaa mbinguni, wanafunzi wake walimwuliza swali kuhusu nini?
․․․․․
▪ Yesu alisema wanafunzi wake wangefanya nini?
․․․․․
ZUNGUMZENI PAMOJA:
Maneno ya malaika katika Matendo 1:11 yametimia jinsi gani? Unaweza kufanya nini ili ushiriki katika kazi ambayo Yesu aliwapa wafuasi wake kama ilivyorekodiwa katika Matendo 1:8?
Katika Toleo Hili
Jibu maswali haya na utaje mistari ya Biblia ambayo haijaonyeshwa.
UKURASA WA 4 Biblia inamfafanuaje Eliya? Yakobo 5:________
UKURASA WA 7 Mwanadamu anapaswa kutegemea nini ili aendelee kuishi? Mathayo 4:________
UKURASA WA 19 Ni nani anayeweza kushikamana kwa ukaribu zaidi kuliko ndugu? Methali 18:________
UKURASA WA 20 Kuna wakati wa kufanya nini? Mhubiri 3:_________
Watoto Watafute Picha
Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.
Ni Nani Aliye Katika Nasaba ya Yesu?
Fikiria madokezo. Soma maandiko. Kisha uandike majina sahihi katika nafasi zilizoonyeshwa.
2 ․․․․․
DOKEZO: Nilipokuwa mfalme, Hilkia alipata “kile kitabu cha sheria ya Yehova kupitia mkono wa Musa.”
Soma 2 Mambo ya Nyakati 34:1, 14.
3 ․․․․․
DOKEZO: Nilikuwa gavana wa kwanza wa Wayahudi waliorudi Israeli kutoka Babiloni.
Soma Hagai 1:14.
4 ․․․․․
DOKEZO: Nilikuwa seremala.
Soma Mathayo 1:16; 13:55.
▪ Majibu kwenye ukurasa wa 14
MAJUBU YA UKURASA WA 31
1. Mlima wa Mizeituni.
▪ Waliuliza Yesu angerudisha Ufalme lini.
▪ Yesu alisema kwamba wanafunzi wake wangekuwa mashahidi wake mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.
2. Yosia.—Mathayo 1:10.
3. Zerubabeli.—Mathayo 1:12.
4. Yosefu.—Mathayo 1:16.
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 31]
Center circle: Oxford Scientific/photolibrary