Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

‘Kitabu Bora Zaidi Kuhusu Dini za Ulimwengu’

‘Kitabu Bora Zaidi Kuhusu Dini za Ulimwengu’

‘Kitabu Bora Zaidi Kuhusu Dini za Ulimwengu’

▪ Mwalimu wa shule ya sekondari nchini Kanada alikabili kipingamizi cha kuwafundisha wanafunzi kuhusu imani za dini mbalimbali katika eneo lake. Baada ya kusoma kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, alisema hivi kwa mshangao: “Hiki ndicho kitabu bora zaidi ambacho nimewahi kusoma kinachoeleza kuhusu dini zilizo ulimwenguni!” Alipendezwa sana hivi kwamba alipokea ruhusa ya halmashauri ya shule ili akitumie darasani.

Mwalimu huyo alisema angeweza kusafiri zaidi ya kilomita 500 ili achukue vitabu 40 kutoka ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova nchini Kanada. Hata hivyo, Mashahidi katika eneo hilo walimpelekea vitabu hivyo. Wanafunzi kadhaa katika darasa hilo walifurahia vitabu hivyo sana hivi kwamba waliomba kupata nakala.

Huenda kitabu hicho kikakusaidia wewe pia kuelewa imani za watu katika jamii yenu. Kinaeleza chanzo, historia, na mafundisho ya dini kubwa za ulimwengu kutia ndani Uhindu, Ubudha, Utao, Ukonfyushasi, Ushinto, Uyahudi, Uislamu, na Ukristo.

Unaweza kuomba kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu chenye picha maridadi kwa kujaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma ukitumia anwani iliyoonyeshwa au anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Bila masharti, ningependa kupokea kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.