Ungejibuje?
Ungejibuje?
Ni Nini Kimekosekana Katika Picha Hii?
Soma 1 Wafalme 18:19-24, 30-40. Kisha utazame picha. Kuna kasoro gani? Andika majibu yako kwenye mistari iliyo hapa chini.
1. ․․․․․
2. ․․․․․
3. ․․․․․
ZUNGUMZENI PAMOJA:
Kwa nini Yehova alikubali dhabihu ya Eliya? Yehova anakubali dhabihu za aina gani kutoka kwa watumishi wake leo?
Katika Toleo Hili
Jibu maswali haya na utaje mistari ya Biblia ambayo haijaonyeshwa.
UKURASA WA 7 Yehova anaitundika dunia wapi? Ayubu 26:________
UKURASA WA 9 Ni kazi za nani zimefanywa kwa hekima? Zaburi 104:________
UKURASA WA 13 Tunachagua uzima kwa kufanya nini? Kumbukumbu la Torati 30:________
UKURASA WA 20 Tunapommiminia Yehova hisia zetu, yeye anatupatia nini? Wafilipi 4:________
Watoto Watafute Picha
Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.
Unajua Nini Kuhusu Manabii?
4. ․․․․․
Ni nabii gani aliyemkaripia Mfalme Yehoashi wa Yuda kwa sababu ya matendo yake maovu?
DOKEZO: Soma 2 Mambo ya Nyakati 24:20-22.
5. ․․․․․
Mfalme Yehoashi aliagiza nabii huyo auawe kwa sababu ya maneno yake. Je, hilo linamaanisha kwamba Yehova hakupendezwa na maneno ya nabii huyo?
DOKEZO: Soma Luka 11:50, 51.
ZUNGUMZENI PAMOJA:
Kwa nini hupaswi kuwa na wasiwasi watu wanapokutesa kwa sababu ya kumtii Yehova?
DOKEZO: Soma Mathayo 5:11, 12 na 1 Petro 4:14.
▪ (Majibu kwenye ukurasa wa 27)
MAJIBU YA UKURASA WA 31
1. Ng’ombe-dume wa kutolewa kuwa dhabihu.
2. Mtaro uliojaa maji.
3. Mamia ya watu waliokuwapo, kutia ndani manabii 450 wa Baali.
4. Zekaria mwana wa Yehoyada.
5. Hapana.