Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wazazi Wanaweza Kusaidia Jinsi Gani?

Wazazi Wanaweza Kusaidia Jinsi Gani?

Wazazi Wanaweza Kusaidia Jinsi Gani?

SHIRIKA moja la elimu nchini Marekani linawahimiza wanafunzi hivi: “Uwe tayari kujikaza kisabuni.” Wakishinikizwa kufikia malengo yao, vijana fulani hujaribu kufanya mengi kuliko uwezo wao wa kimwili. Madeline Levine, aliyetajwa katika makala iliyotangulia, aliandika hivi: “Wakiwa wamesongwa na mambo mengi kama vile, masomo yatakayowasaidia kutimiza mengi zaidi, utendaji mwingi wa baada ya shule, masomo ya kujitayarishia kujiunga na shule za sekondari au chuo, na walimu wanaolipwa kuwasaidia wafaulu katika masomo, vijana wengi wanakuwa na shughuli nyingi sana hivi kwamba wanahatarisha maisha yao.” Wanafunzi walio katika hali hiyo wanaweza kupatwa na madhara ya kimwili na kihisia.

Ikiwa una wasiwasi kuhusu mfadhaiko ambao mtoto wako anakabili shuleni, nenda shuleni wewe mwenyewe. Zungumza na walimu, washauri, na wasimamizi. Waambie mambo ambayo umeona katika mtoto wako. Una haki ya kufanya hivyo.

Biblia inawatia moyo wazazi wakazie uangalifu maendeleo ambayo watoto wao wanafanya kadiri wanavyokua. Musa aliwaambia hivi wazazi katika taifa la Israeli: ‘Nawe ukazie sheria ya Mungu kwa mwana wako na kuisema unapoketi katika nyumba yako na unapotembea barabarani na unapolala na unapoamka.’—Kumbukumbu la Torati 6:7.

Kupendezwa sana na elimu ya mtoto wako si kuingilia faragha yake. Inaonyesha kwamba unamuunga mkono mtoto wako. Na kufanya hivyo kunaweza kupunguza sana mfadhaiko ambao mtoto wako anapata shuleni.

[Picha katika ukurasa wa 8, 9]

Zungumza na walimu na washauri wa shule kuhusu mfadhaiko wa mtoto wenu