Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Unaweza Kufanya Nini Ili Uokoke Mwisho wa Ulimwengu?”

“Unaweza Kufanya Nini Ili Uokoke Mwisho wa Ulimwengu?”

“Unaweza Kufanya Nini Ili Uokoke Mwisho wa Ulimwengu?”

▪ Biblia inamaanisha nini inapozungumzia mwisho wa dunia au wa mfumo wa mambo wa sasa? Je, inamaanisha kutakuwa na vita vya nyuklia vitakavyofagilia mbali wanadamu wote? Au je, inamaanisha kutakuwa na msiba wa asili kama vile dunia kugongwa na sayari ndogo? Kwa kupendeza, Biblia inasema kwamba “umati mkubwa” wa wanadamu utaokoka mwisho wa dunia. (Ufunuo 7:9, 10, 14) Ni nani hao watakaookoka? Je, unaweza kuwa miongoni mwao?

Maswali hayo muhimu yatajibiwa katika hotuba ya watu wote “Unaweza Kufanya Nini Ili Uokoke Mwisho wa Ulimwengu?” Hotuba hiyo itatolewa kwenye makusanyiko ya “ENDELEENI KUKESHA!” ya Mashahidi wa Yehova, yatakayofanywa kuanzia Mei nchini Marekani na kuendelea ulimwenguni pote. Unaalikwa kwa uchangamfu uhudhurie kusanyiko litakalofanywa karibu na mahali unapoishi. Wasiliana na Mashahidi wa Yehova katika eneo lenu au waandikie barua wachapishaji wa gazeti hili. Gazeti la Mnara wa Mlinzi la Machi 1, 2009 (1/3/2009), lina orodha ya mahali ambapo makusanyiko yote yatafanywa nchini Burundi, Kenya, Kongo (Kinshasa), Malawi, Rwanda, Tanzania, na Uganda.