Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Siri ya 2: Kuwajibika

Siri ya 2: Kuwajibika

Siri ya 2: Kuwajibika

“Kile ambacho Mungu ameunganisha mtu yeyote asikitenganishe.”—Mathayo 19:6.

Hilo linahusisha nini? Wenzi wa ndoa wenye mafanikio huona ndoa yao kuwa muungano wa kudumu. Tatizo linapotokea, wao hujaribu kulisuluhisha badala ya kulitumia kama kisababu cha kuvunja ndoa yao. Wenzi wa ndoa wanapowajibika, wao hujihisi salama. Kila mmoja huamini kwamba mwenzake ataendelea kuheshimu ndoa yao.

Kwa nini ni muhimu? Kwa njia nyingi, kuwajibika ndio msingi wa ndoa. Hata hivyo, baada ya kuzozana mara nyingi, kuwajibika kunaweza kuonekana kama mtego badala ya kuwa jambo la hiari. Kwa sababu hiyo, maneno “mpaka kifo kitutenganishe” huenda yasimaanishe jambo lolote la maana, kwani wenzi wa ndoa wanaweza kuwa wakitafuta visababu vya kutoka kwenye mkataba huo. Huenda wasivunje ndoa yao kihalisi, lakini wanaweza kujitenga kwa njia nyingine. Kwa mfano, wanaweza kunyamaza kimya wakati matatizo mazito yanapohitaji kuzungumziwa.

Jaribu kufanya hivi. Jaribu kupima unawajibika kadiri gani kwa familia yako kwa kutumia maswali yafuatayo.

Tunapozozana, je, mimi hujikuta nikijuta kwamba nilifunga ndoa na mwenzi wangu?

Je, mimi hujiwazia nikiwa na mtu mwingine ambaye si mwenzi wangu?

Je, nyakati nyingine mimi humwambia mwenzi wangu, “Ninakuacha” au “Nitatafuta mtu anayenithamini”?

Azimia. Fikiria jambo moja au mawili ambayo unaweza kufanya ili kuwajibika zaidi. (Madokezo: Ili kuonyesha kwamba unamfikiria, mara kwa mara mwandikie mwenzi wako barua fupi, weka picha zake mahali palipo wazi kazini, au mpigie simu kila siku kutoka kazini.)

Mbona usifikirie mambo mengine kisha umwulize mwenzi wako ni mambo gani ambayo yatampendeza zaidi?

[Picha katika ukurasa wa 4]

Kuwajibika kunalinda ndoa yako kama tu vyuma vilivyo kando ya barabara vinavyolinda magari yasitoke barabarani

[Hisani]

© Corbis/age fotostock