Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Kushinda Mwelekeo wa Kuwa na Ubinafsi”

“Kushinda Mwelekeo wa Kuwa na Ubinafsi”

“Kushinda Mwelekeo wa Kuwa na Ubinafsi”

● GIBRALTAR, ambayo iko kusini kabisa ya Rasi ya Iberia, imezingirwa na kuvamiwa mara nyingi sana. Lakini kwenye mwisho wa juma moja, mwezi wa Oktoba (Mwezi wa 10) 2008, mji huo “ulivamiwa” na Wahispania 1,000 hivi wenye amani. Walienda huko kujenga Jumba la Ufalme ambalo lingetumiwa na makutaniko mawili ya Mashahidi wa Yehova huko Gibraltar.

Waziri mkuu wa serikali alimwambia mwandishi wa Amkeni! kwamba watu wote hao 1,000 hivi walioenda huko Gibraltar kwa ajili ya kazi hiyo walikaribishwa. Alisema kwamba “wanachangia kuboreshwa kwa jamii.” Alisema kwamba “kikundi hicho cha Mashahidi wa Yehova ndicho kikundi kikubwa sana cha watu kuja kufanya kazi katika mradi mmoja, na jambo la kushangaza hata zaidi ni kwamba ulikuwa mradi wa kujitolea.”

Wenye mamlaka wa eneo hilo waliunga mkono mradi huo tangu mwanzo na kuwapa Mashahidi eneo linalofaa kwa ajili ya ujenzi wa jengo hilo la ibada. Ni nini kilichowachochea wenye mamlaka kuwa wakarimu hivyo?

“Ninaamini kwamba ni muhimu kwa jamii yoyote ile kumpenda Mungu,” akasema waziri huyo mkuu. “Kulingana na katiba, dini zote huku Gibraltar zina uhuru wa ibada, kwa hiyo, serikali haipaswi kubagua dini yoyote. Isitoshe, kuandaa uwanja unaofaa kwa ajili ya Mashahidi kujenga mahali pa kuabudu ni kwa faida ya jamii yetu.

“Tunahitaji kushinda mwelekeo wa kuwa na ubinafsi,” akaendelea kusema. “Kikundi chenu cha wajitoleaji wenye uchangamfu kimeonyesha kwamba jambo hilo linawezekana.”

Licha ya kwamba dhoruba ilizuia kazi isianze, Jumba la Ufalme lilikamilishwa Jumatatu (Siku ya 1), siku ya tatu ya mradi huo. “Wajitoleaji wengi waliamua kubaki Gibraltar ili wakamilishe mradi huo,” akasema Secundino Nogal, ambaye alisimamia kazi hiyo. “Tumezoea kukabiliana na matatizo. Mbinu yetu ya ujenzi inahitaji tuwe tayari kubadilikana. Lakini zaidi ya yote, mtu hapaswi kuwa na ubinafsi, na ndiyo sababu kazi yetu inaturidhisha sana.” *

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 7 Gazeti la eneo hilo Gibraltar Chronicle, liliripoti hivi: “Kwenye mwisho wa juma ambao dhoruba ilisababisha uharibifu mwingi sana, Mashahidi wa Yehova wa Gibraltar . . . walikamilisha ujenzi wa hekalu lao [Jumba la Ufalme] katika muda wa siku tatu tu kwa msaada wa jeshi kubwa la wajitoleaji.”