Mazungumzo ya Familia
Mazungumzo ya Familia
Je, Ulikuwa Uamuzi Mzuri?
Soma Mwanzo 39:1-23. Sasa tazama picha, na uandike majibu yako kwenye mistari iliyo hapo chini.
1. Mwanamke aliye katika picha hii ni nani?
․․․․․
2. Mwanamume huyo ni nani?
․․․․․
3. Mwanamume huyo alifanya uamuzi gani?
․․․․․
ZUNGUMZENI PAMOJA:
Kwa nini mwanamume huyo alifanya uamuzi huo? Je, ulimuumiza? Je, unafikiri alifanya uamuzi unaofaa, na ikiwa ndivyo, kwa nini unafikiri hivyo? Ni wakati gani unaweza kuumia kwa sababu ya kufanya jambo linalofaa?
UNAJUA NINI KUHUSU MFALME SAULI?
4. Ni mambo gani yaliyomfanya Sauli awe mwenye kuvutia?
DOKEZO: Soma 1 Samweli 9:1, 2.
․․․․․
5. Kwa nini Yehova alimkataa Sauli?
DOKEZO: Soma 1 Samweli 13:13, 14.
․․․․․
ZUNGUMZENI PAMOJA:
Ni nini kilicho muhimu kwa Mungu kuliko sura ya mtu?
DOKEZO: Soma 1 Samweli 16:6, 7.
Kujua jambo hilo kunaweza kukusaidia jinsi gani kuwa na maoni yenye usawaziko kuhusu sura yako?
DOKEZO: Soma 1 Timotheo 4:8.
WATOTO WATAFUTE PICHA
Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.
KATIKA TOLEO HILI
Jibu maswali haya, na utaje mistari ya Biblia ambayo haijaonyeshwa.
UKURASA WA 4 Biblia inatuambia nini kuhusu kazi? Mhubiri 3:________
UKURASA WA 7 Tunapaswa kufanya kazi kwa kusudi gani? Yohana 6:________
UKURASA WA 10 Mungu ameweka siku ya kufanya nini? Matendo 17:________
UKURASA WA 28 Watu wanapooana wanakuwa nini? Mwanzo 2:________
● Majibu kwenye ukurasa wa 14
MAJIBU YA UKURASA WA 31
1. Mke wa Potifa.
2. Yosefu.
3. Alikataa kulala na mke wa Potifa.
4. Sauli alikuwa mrefu na mwenye sura nzuri.
5. Sauli hakumtii Mungu.