Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Yesu Alitoa Uhai Wake kwa Ajili ya Wengi

Yesu Alitoa Uhai Wake kwa Ajili ya Wengi

Yesu Alitoa Uhai Wake kwa Ajili ya Wengi

Yesu Kristo aliwaambia wafuasi wake kwamba alikuja duniani, “si kuhudumiwa, bali kuhudumu na kutoa nafsi yake kuwa fidia badala ya wengi.” (Mathayo 20:28) Alitoa uhai wake kwa hiari kwa faida ya wengine.

Yesu aliandaa fidia jinsi gani kupitia kifo chake? Kwa nini ilihitajika? Yesu alitoa uhai wake kwa ajili ya nani? Na kifo chake kinaweza kumaanisha nini kwako?

Mashahidi wa Yehova wanakukaribisha kwa uchangamfu ujiunge nao kuchunguza majibu ya Biblia ya maswali hayo. Mwaka huu, Ukumbusho wa kifo cha Yesu utafanywa Jumanne (Siku ya 2), Machi 30 baada ya jua kushuka. Pindi hiyo, majibu ya Biblia ya maswali yaliyo hapo juu yatatolewa.

Unaweza kuhudhuria tukio hilo kwenye Jumba la Ufalme lililo karibu na nyumbani kwako. Tafadhali wasiliana na Mashahidi wa Yehova walio karibu na kwenu wakueleze wakati na mahali litakapofanyiwa.