Mazungumzo ya Familia
Mazungumzo ya Familia
Je, Ulikuwa Uamuzi Mzuri?
Soma Marko 14:66-72. Sasa tazama picha, na uandike majibu yako kwenye mistari iliyo hapo chini.
1. Tukio hili katika picha lilifanyika wapi?
DOKEZO: Soma Marko 14:53, 54.
․․․․․
2. Petro aliamua kufanya nini alipoambiwa kwamba yeye ni mfuasi wa Yesu?
․․․․․
3. Ni nini kilichotokea baada ya jogoo kuwika mara ya pili?
․․․․․
ZUNGUMZENI PAMOJA:
Unafikiri ni kwa nini Petro alitenda kwa njia hiyo? Unaweza kuepuka kufanya kosa kama hilo jinsi gani?
UNAJUA NINI KUHUSU MFALME YEHOSHAFATI?
4. Yehoshafati aliboresha mfumo wa sheria wa Yuda jinsi gani?
DOKEZO: Soma 2 Mambo ya Nyakati 19:5-11.
․․․․․
5. Yehoshafati alifanya kosa gani?
DOKEZO: Soma 2 Mambo ya Nyakati 18:1-3; 19:1-3.
․․․․․
ZUNGUMZENI PAMOJA:
Kutokana na simulizi la Yehoshafati, unaweza kujifunza nini kuhusu kuchagua marafiki?
DOKEZO: Soma 1 Wakorintho 15:33.
WATOTO WATAFUTE PICHA
Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.
KATIKA TOLEO HILI
Jibu maswali haya, na utaje mistari ya Biblia ambayo haijaonyeshwa.
UKURASA WA 4 Tunapaswa kujisafisha wenyewe kutokana na nini? 2 Wakorintho 7:________
UKURASA WA 5 Watu wawili wanaweza kutimiza nini? Mhubiri 4:________
UKURASA WA 19 Watu wenye hekima hawategemei nini? 1 Timotheo 6:________
UKURASA WA 27 Utakuwa mwenye furaha zaidi unapofanya nini? Matendo 20:________
● Majibu kwenye ukurasa wa 24
MAJIBU YA UKURASA WA 31
1. Kwenye ua wa nyumba ya kuhani mkuu.
2. Petro aliamua kukana kwamba anamjua Yesu.
3. Petro alilia.
4. Yehoshafati aliwateua waamuzi wanaomwogopa Mungu katika majiji na pia akawaweka rasmi Walawi na makuhani huko Yerusalemu.
5. Alifanya mapatano na Mfalme Ahabu mwovu.