Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Unaweza Kumkaribia Mungu Jinsi Gani?

Unaweza Kumkaribia Mungu Jinsi Gani?

Unaweza Kumkaribia Mungu Jinsi Gani?

Biblia inasema: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.” (Yakobo 4:8) Je, unaamini kwamba wanadamu wanaweza kuwa na uhusiano mzuri, wa karibu pamoja na Muumba wao? Kabla ya kujibu swali hilo, unahitaji kupata majibu yanayofaa kwa maswali ya msingi zaidi. Kwa mfano:

Je, kuna Mungu?

Ikiwa yuko, je, amewasiliana na wanadamu? Kwa njia gani?

Je, Biblia ni uthibitisho wa kwamba Mungu amewasiliana nasi? Tunaweza kuwa na uhakika jinsi gani?

Huenda haya ndiyo maswali muhimu zaidi tunayoweza kujiuliza, na yatazungumziwa katika hotuba ya watu wote yenye kichwa “Unaweza Kumkaribia Mungu Jinsi Gani?” Itatolewa katika Makusanyiko ya Wilaya ya Mashahidi wa Yehova yenye kichwa, “Kaa Karibu na Yehova!” Makusanyiko hayo yataanza Mei (Mwezi wa 5) kule Marekani na kuendelea ulimwenguni pote.

Unaalikwa kwa moyo mkunjufu uhudhurie kusanyiko litakalofanywa karibu na mahali unapoishi. Kwa habari zaidi, tafadhali wasiliana na Mashahidi wa Yehova katika eneo lenu au waandikie barua wachapishaji wa gazeti hili. Gazeti la Mnara wa Mlinzi la Machi 1, 2010 na Tovuti ya www.pr418.com ina orodha ya mahali ambapo makusanyiko yote yatafanywa nchini Burundi, Kenya, Kongo (Kinshasa), Malawi, Rwanda, Tanzania, na Uganda.