Mazungumzo ya Familia
Mazungumzo ya Familia
Ni Nani Aliyefanya Kazi Hii?
1. Ni wavuvi gani wawili waliokuwa wana wa Zebedayo na pia walikuwa mitume wa Yesu?
Andika majibu yako katika mstari ulio chini.
DOKEZO: Soma Mathayo 4:21, 22.
․․․․․
2. Andika majina ya mitume wengine wawili ambao pia walikuwa wavuvi.
DOKEZO: Soma Mathayo 4:18.
․․․․․
ZUNGUMZENI PAMOJA:
Kwa nini Yesu alisema kwamba wanafunzi wake wangekuwa “wavuvi wa watu”? (Mathayo 4: 19) Unafikiri kuvua samaki na kuvua watu kunafanana katika njia gani? Kunatofautiana jinsi gani?
UNAJUA NINI KUHUSU MTUME ANDREA?
3. Kabla ya kumfuata Yesu, Andrea alikuwa mwanafunzi wa nani?
DOKEZO: Soma Marko 1:4; Yohana 1:35-40.
․․․․․
4. Andrea alimweleza nani kumhusu Yesu, na matokeo yakawa nini?
DOKEZO: Soma Yohana 1:40-42.
․․․․․
ZUNGUMZENI PAMOJA:
Kwa nini ni jambo zuri kuwaeleza watu wako wa ukoo mambo unayojua kumhusu Yesu? Lakini, huenda baadhi yao wakaitikia namna gani?
DOKEZO: Soma Mathayo 10:32-37.
WATOTO WATAFUTE PICHA
Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.
KATIKA TOLEO HILI
Jibu maswali haya, na utaje mistari ya Biblia ambayo haijaonyeshwa.
UKURASA WA 3 Mtu mwerevu hufikiria nini? Methali 14:________
UKURASA WA 8 Mungu alijipatia jina gani la kibinafsi? Zaburi 83:________
UKURASA WA 20 Malaika waliotenda dhambi wamepatwa na nini? Yuda:________
UKURASA WA 26 “Kuchochea hasira” hutokeza nini? Methali 30:________
● Majibu kwenye ukurasa wa 11
MAJIBU YA UKURASA WA 31
1. Yakobo na Yohana.
2. Petro na Andrea.
3. Yohana Mbatizaji.
4. Petro ndugu yake, ambaye baadaye alikuwa mwanafunzi wa Yesu.