Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Je, Ulikuwa Uamuzi Mzuri?

Soma Marko 12:41-44. Sasa tazama picha, na uandike majibu yako kwenye mistari iliyo hapo chini.

1. Masanduku ya hazina yalikuwa wapi?

DOKEZO: Soma Marko 12:35; 13:1.

․․․․․

2. Ingawa mjane alitoa kiasi kidogo cha mchango, kwa nini Yesu alimsifu?

DOKEZO: Soma Marko 12:28-30.

․․․․․

3. Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba mjane huyo hakuteseka, ingawa alitoa “riziki yake yote”?

DOKEZO: Soma Mathayo 6:25, 31-33.

․․․․․

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Unafikiri mjane huyo alifanya uamuzi mzuri? Kwa nini unasema hivyo? Utapata matokeo gani ikiwa utakuwa na zoea la kutoa kwa ukarimu?

DOKEZO: Soma Luka 6:38; Matendo 20:35.

UNAJUA NINI KUHUSU MTUME YOHANA?

4. Je, viongozi wa kidini walimwona Yohana kuwa msomi na msemaji?

DOKEZO: Soma Matendo 4:13.

․․․․․

5. Yohana alipewa pendeleo gani la pekee?

DOKEZO: Soma Ufunuo 1:1-3.

․․․․․

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Yohana aliandika vitabu vingapi vya Biblia? Unaweza kumwiga Yohana kwa njia gani?

WATOTO WATAFUTE PICHA

Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.

KATIKA TOLEO HILI

Jibu maswali haya, na utaje mistari ya Biblia ambayo haijaonyeshwa.

UKURASA WA 9 Kuna furaha zaidi katika kufanya nini? Matendo 20:________

UKURASA WA 9 Ni nini kinachowatambulisha wanafunzi wa Yesu? Yohana 13:________

UKURASA WA 21 Amani ya Mungu inaweza kufanya nini? Wafilipi 4:________

UKURASA WA 22 Yehova yuko karibu na nani? Zaburi 34:________

● Majibu kwenye ukurasa wa 21

MAJIBU YA UKURASA WA 31

1. Ndani ya hekalu.

2. Mjane alimpa Mungu kila kitu alichokuwa nacho.

3. Mungu anaahidi kututunza ikiwa tutatanguliza mambo ya Ufalme.

4. La. Walimwona Yohana kuwa mtu asiye na elimu na wa kawaida tu.

5. Aliongozwa na roho ya Mungu kuandika sehemu fulani za Biblia, kutia ndani kitabu cha Ufunuo.