Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Alijifunza Wakati Mmoja na Watoto Wake

Alijifunza Wakati Mmoja na Watoto Wake

Alijifunza Wakati Mmoja na Watoto Wake

Mama mmoja mwenye umri wa miaka 30 na kitu anayeishi pamoja na mume wake na watoto wao watatu huko Kentucky, Marekani, aliandika, “Mimi pamoja na familia yangu tumefaidika kwa kusoma vichapo vinavyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.” Anaeleza: “Watoto wangu wanapenda sana Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia,” kisha anaongezea, “Nilijifunza wakati mmoja na watoto wangu.”

Kitabu hicho kina picha zenye kupendeza na kinazungumzia matukio ya Biblia kulingana na wakati yalipotukia. Kwa mfano: Sehemu ya 2 inatia ndani hadithi kama vile “Mfalme Mbaya Anatawala Misri,” “Namna Mtoto Musa Alivyookolewa,” “Sababu Musa Alikimbia,” “Musa na Haruni Wanamwona Farao,” “Mapigo 10,” na “Kuvuka Bahari Nyekundu (ya Shamu).”

Sehemu ya 6 ya kitabu hicho yenye kichwa, “Kuzaliwa Yesu Mpaka Kufa Kwake,” ina hadithi nyingi kuhusu maisha ya Yesu tangu kuzaliwa kwake hadi kifo chake. Baadhi ya hadithi hizo ni “Yesu Anazaliwa Katika Boma la Ng’ombe” na “Wanaume Walioongozwa na Nyota.” Hadithi hiyo ya mwisho inaonyesha kwamba wale “mamajusi,” ambao kwa kweli walikuwa wanajimu walimtembelea Yesu ‘ndani ya nyumba’ wala si katika hori alipozaliwa. Wakiwa ndani ya nyumba ‘walimwona huyo mtoto mchanga pamoja na Maria mama yake.’ Wanaume hao walionywa na Mungu wasirudi kwa Herode ambaye alitaka kumwua Yesu. Jambo hilo linatuonyesha nini kuhusu nyota ambayo iliwaongoza?—Mathayo 2:1, 11, 12.

Wewe pia unaweza kujifunza mambo fulani wakati mmoja na watoto wako unaposoma Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Kina hadithi 116 ambazo zinazungumzia watu na matukio ya Biblia. Unaweza kuomba kitabu hicho kwa kujaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma ukitumia anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Bila masharti, ningependa kupokea kitabu kilichoonyeshwa hapa.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.