Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Ni Nini Kimekosekana Katika Picha Hii?

Soma 2 Wafalme 4:8-10. Kisha utazame picha. Ni vitu gani vimekosekana? Andika majibu yako kwenye mistari iliyo hapa chini. Unganisha nukta zilizopo ili ukamilishe picha hii, kisha uipake rangi.

1. ․․․․․

2. ․․․․․

3. ․․․․․

[Mchoro]

(Ona nakala iliyochapishwa)

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Mwanamke huyu alionyesha fadhili jinsi gani? Ni kwa njia gani Yehova alibariki matendo yake ya fadhili kwa sababu ya kumtegemeza nabii wake?

DOKEZO: Soma 2 Wafalme 4:32-37.

Ni kwa njia gani unaweza kuwaonyesha watumishi wa Yehova fadhili leo?

DOKEZO: Soma Waroma 12:13; Wagalatia 6:10.

UTENDAJI WA FAMILIA:

Bila kusema jambo lolote, mshiriki mmoja wa familia anaweza kuigiza sehemu ya mtu mmoja katika simulizi la Biblia lililotajwa hapo juu. Wengine katika familia wajaribu kukisia mtu huyo ni nani.

Kusanya na Ujifunze

Kata, kunja katikati, na uhifadhi

KADI YA BIBLIA 2 DANIELI

MASWALI

A. Kwa nini Danieli alitupwa katika shimo la simba?

B. Rafiki watatu wa Danieli walikuwa na majina gani ya Kiebrania?

C. Danieli alitumikia chini ya falme gani mbili za kigeni?

[Chati]

4026 K.W.K. 1 W.K. 98 W.K.

Adamu aumbwa Aliishi miaka Kitabu cha mwisho cha

ya 600 K.W.K. Biblia kinaandikwa

[Ramani]

Alichukuliwa kutoka Yerusalemu hadi Babiloni

Yerusalemu

Babiloni

DANIELI

MAMBO MACHACHE KUMHUSU

Huenda alikuwa mwana wa mfalme, alizaliwa katika kabila la Yuda. Alikuwa nabii mwaminifu aliyeongozwa na roho ya Mungu kuandika kitabu kilichoitwa kwa jina lake. Huenda Danieli alikuwa kijana wakati yeye na watu wengine wa familia ya kifalme na wakuu walipochukuliwa mateka na Nebukadneza hadi Babiloni.

MAJIBU

A. Alisali kwa Yehova ingawa aliamriwa asifanye hivyo.—Danieli 6:6-17.

B. Hanania, Mishaeli, Azaria.—Danieli 1:6, 7.

C. Babiloni na Muungano wa Umedi na Uajemi.—Danieli 5:30; 6:8.

Watu na Nchi

4. Majina yetu ni Jorge, Nicolas, na Priscilian. Tunaishi nchini Belize, katika Amerika ya Kati. Kuna Mashahidi wangapi wa Yehova nchini Belize? Ni 600, 2,000, au 3,500?

5. Ni alama gani inayoonyesha eneo ninaloishi? Chora duara kuzunguka alama hiyo, na uchore alama nyingine kuonyesha eneo unaloishi kisha uone kwenu ni umbali gani kutoka Belize.

A

B

C

D

Watoto Watafute Picha

Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.

● Majibu ya ukurasa wa 30 na 31 kwenye ukurasa wa 28

MAJIBU YA UKURASA WA 30 NA 31

1. Kitanda.

2. Meza.

3. Kiti.

4. 2,000.

5. A.