Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wao Si Wachanga Sana

Wao Si Wachanga Sana

Wao Si Wachanga Sana

● Hivyo ndivyo mama mmoja huko California, Marekani, alivyoandika kuhusu jambo linalozungumziwa katika kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Alieleza hivi: “Juma lililopita mwana wetu Javan, mwenye umri wa miaka 3, alienda kwa daktari, na daktari huyo akauliza ikiwa mimi na mume wangu tumemfundisha Javan kuhusu jinsi ya kulinda sehemu zake za siri. Nilifurahi kumweleza kuhusu kitabu Mwalimu, kinachoeleza kwamba ni vibaya kwa mtu yeyote kuchezea sehemu za siri za mtu mwingine. Daktari huyo alifurahi sana kwamba tulikuwa tumezungumzia jambo hilo.”

Mama huyo alisema hivi pia: “Kitabu hicho kinazungumzia mambo hayo kwa njia nzuri kabisa.” Sura ambayo mama huyo alikuwa akizungumzia ina kichwa “Jinsi Yesu Alivyolindwa.” Inafafanua jinsi Baba wa mbinguni wa Yesu alivyomlinda Mwana wake asiumizwe na Mfalme Herode wakati Yesu alipokuwa mchanga asiweze kujilinda. (Mathayo 2:7-23) Kitabu hicho kinaonyesha pia jinsi watoto wachanga wanavyoweza kufundishwa kujilinda mtu anapojaribu kuwatendea vibaya kingono.

Unaweza kuomba nakala ya kitabu hicho kilicho na kurasa 256 na picha zenye kuvutia kilicho na ukubwa kama wa gazeti hili. Tafadhali jaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma ukitumia anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

Bila masharti, ningependa kupokea kitabu kilichoonyeshwa hapa.

Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.