Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Asanteni kwa Kunionyesha Baba Mwenye Upendo”

“Asanteni kwa Kunionyesha Baba Mwenye Upendo”

“Asanteni kwa Kunionyesha Baba Mwenye Upendo”

● Msichana mmoja mwenye umri wa miaka 19 kutoka kusini mwa Marekani aliandika hivi: “Nililelewa katika familia iliyoenda kanisani kwa ukawaida na nimemkubali Kristo kuwa Mwokozi wa maisha yangu. Hata hivyo, kwa miaka mingi nimeishi nikiwa na hofu kwamba Mungu atanihukumu kuwa ninastahili kuteseka katika moto wa mateso. Kisha nikaanza kusoma kitabu chenu Biblia Inafundisha Nini Hasa?

“Baada tu ya kusoma sura kadhaa, nilihisi nikiwa na amani nyingi. Nilihisi ni kana kwamba ndovu alikuwa ameondolewa kutoka kifuani mwangu. Sasa nimekuja kuona kwamba Yehova ni Mungu mwenye upendo, fadhili, na mwenye rehema. Anataka niwe na uhusiano pamoja naye bila kumwogopa. Ninapanga kwenda kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova Jumapili (Siku ya Yenga) hii! Nina furaha sana. Asanteni kwa kunionyesha Baba mwenye upendo na si yule aliyeumba moto wa mateso.”

Kitabu Biblia Inafundisha kinazungumzia pia mambo mengine muhimu. Yanatia ndani hali ya wafu, tumaini la ufufuo, jinsi ya kuboresha maisha ya familia, ukweli kumhusu Mungu na Yesu Kristo, na kwa nini Mungu anaruhusu kuteseka. Unaweza kuomba nakala ya kitabu hicho kwa kujaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma ukitumia anwani ifaayo katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

Bila masharti ningependa kupokea kitabu kilichoonyeshwa.

Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.