Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Yesu “Huondolea Mbali Dhambi ya Ulimwengu”

Yesu “Huondolea Mbali Dhambi ya Ulimwengu”

Yesu “Huondolea Mbali Dhambi ya Ulimwengu”

● Yohana Mbatizaji alisema kwamba Yesu “huondolea mbali dhambi ya ulimwengu.” (Yohana 1:29) Hilo linakazia fungu la Yesu katika kuwaokoa wanadamu watiifu.

Lakini, kwa nini Yesu alihitajika kufa ili kuokoa watenda dhambi? Alitimiza nini kwa kutoa uhai wake kwa hiari? Ni nani wanaofaidika na kifo chake? Kifo chake kina umuhimu gani kwako?

Kila mwaka, Mashahidi wa Yehova hukusanyika kuadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Yesu. Mwaka huu, Ukumbusho huo utafanywa Jumapili (Siku ya Yenga), Aprili (Mwezi wa 4) 17, baada ya jua kutua.

Mashahidi wa Yehova wanakualika kwa uchangamfu ujiunge nao katika kuchunguza umuhimu wa kifo cha Yesu. Maswali yaliyo hapo juu yatajibiwa kwa kutumia Biblia.

Unaweza kuhudhuria tukio hilo karibu na nyumbani kwako. Tafadhali wasiliana na Mashahidi wa Yehova wa eneo lako ili wakueleze wakati na mahali litakapofanyiwa.