Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Midomo Yako Ni “Vyombo Vyenye Thamani”?

Je, Midomo Yako Ni “Vyombo Vyenye Thamani”?

Je, Midomo Yako Ni “Vyombo Vyenye Thamani”?

● “Kuna dhahabu, pia kuna wingi wa marijani; lakini midomo ya ujuzi ni vyombo vyenye thamani,” akaandika Mfalme Sulemani wa kale. (Methali 20:15) Tangu zamani dhahabu imekuwa kitu chenye thamani sana, na katika siku za Sulemani, marijani pia yalionwa kuwa yenye thamani. Hata hivyo, midomo yetu inaweza kuwa yenye thamani hata zaidi kuliko vitu hivyo. Jinsi gani? Si kwa sababu ya urembo wake, bali kwa sababu ya maneno inayosema.

Midomo yenye thamani husema maneno mema, yenye fadhili, na upendo. Na “midomo ya ujuzi,” husema ukweli kumhusu Mungu kama ilivyoandikwa kwenye Biblia. Ndiyo, kitabu hicho cha kale kimejaa hekima na ukweli kumhusu Muumba wetu, na vilevile mashauri yanayofaa kuhusu maisha.—Yohana 17:17.

Hata hivyo, inasikitisha kwamba watu wengi hutumia midomo yao vibaya kwa kusema mambo yasiyo ya kweli kumhusu Mungu. Kwa mfano, watu fulani humlaumu kwa sababu ya ukosefu wa haki na kuteseka ulimwenguni, ingawa mengi ya mambo hayo husababishwa na wanadamu. Kwa sababu hiyo, Methali 19:3 inasema hivi: “Mtu akijiangamiza kwa upumbavu wake, huielekeza hasira yake dhidi ya Mwenyezi-Mungu.”—Biblia Habari Njema.

Wengine pia hupunguza thamani ya midomo yao kwa kusambaza habari zisizo za kweli, porojo yenye kuumiza, au hata uchongezi. Kwa kutumia mfano wenye nguvu, andiko la Methali 26:23 linasema hivi: “Kama fedha inayofunika kipande cha chombo cha udongo, ndivyo ilivyo midomo yenye bidii pamoja na moyo mbaya.” Kama “fedha inayofunika” ifichavyo udongo, ndivyo “midomo yenye bidii,” ambayo inamaanisha hisia zenye nguvu na hata unyoofu, inavyoweza kuficha “moyo mbaya.”—Methali 26:24-26.

Kwa hakika, uovu kama huo uko wazi mbele ya macho ya Mungu. Anaona jinsi tulivyo kwa kweli! Hivyo, Yesu Kristo alisema hivi: “Kwanza safisha upande wa ndani wa kikombe na wa sahani, ili upande wake wa nje upate kuwa safi pia.” (Mathayo 23:26) Hilo ni kweli kabisa! Zaidi ya hilo, ikiwa tutakuwa na moyo safi uliojaa kweli za Neno la Mungu, itaonekana wazi kupitia yale tunayosema. Matokeo yatakuwa nini? Midomo yetu itakuwa “vyombo vyenye thamani,” hasa machoni pa Mungu.

[Picha katika ukurasa wa 19]

Midomo ya mwenye hekima ni “vyombo vyenye thamani”