Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Mazungumzo ya Familia

Ni Nini Kimekosekana Katika Picha Hii?

Soma Mwanzo 13:5-17. Kisha utazame picha. Ni vitu gani vimekosekana? Andika majibu yako kwenye mistari iliyo hapa chini. Unganisha nukta zilizopo ili ukamilishe picha hii, kisha uipake rangi.

1. ․․․․․

2. ․․․․․

[Mchoro]

(Ona nakala iliyochapishwa)

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Ni ubishi gani uliotokea kati ya Loti na Abrahamu na wachungaji wa wanyama wao? Abrahamu alifanya amani jinsi gani ingawa alikuwa na haki fulani akiwa kichwa cha familia?

DOKEZO: Soma Mwanzo 13:7-9.

Je, Abrahamu alimwekea Loti kinyongo?

DOKEZO: Soma Mwanzo 14:12-16.

Abrahamu alithawabishwa jinsi gani kwa sababu ya sifa zake za kimungu?

DOKEZO:? Soma Mwanzo 13:14-17.

Unaweza kuonyesha jinsi gani kwamba wewe ni mfanya-amani?

DOKEZO: Soma 1 Wakorintho 13:4, 5; Yakobo 3:13-18.

UTENDAJI WA FAMILIA:

Bila kusema jambo lolote, mtu mmoja wa familia anaweza kuigiza sehemu ya mtu mmoja katika simulizi la Biblia lililotajwa hapo juu. Wengine katika familia wajaribu kukisia mtu huyo ni nani.

Kusanya na Ujifunze

Kata, kunja katikati, na uhifadhi

KADI YA BIBLIA 5 ABRAHAMU

MASWALI

A. Abrahamu alikuwa na umri wa miaka mingapi mwana wake Isaka alipozaliwa?

B. Yehova alimpa Abrahamu ahadi gani?

C. Jaza mapengo. Kwa sababu ya kazi na imani yake kubwa, Abrahamu alikuja kuitwa ______________.

[Chati]

4026 K.W.K. 1 W.K. 98 W.K.

Adamu aumbwa Aliishi Kitabu cha

Miaka ya 1900 K.W.K. mwisho cha Biblia chaandikwa

[Ramani]

Alihama kutoka Uru hadi Kanaani

Uru

Harani

KANAANI

ABRAHAMU

MAMBO MACHACHE KUMHUSU

Mwanamume mwaminifu aliyehama kutoka jiji la Uru lililokuwa limesitawi ili atimize mapenzi ya Yehova, ingawa hakujua mahali ambapo angeishi. (Waebrania 11:8-10) Sikuzote alifundisha familia yake “washike njia ya Yehova ili kutenda uadilifu.” (Mwanzo 18:19) Biblia inamwita “baba ya wale wote walio na imani.”—Waroma 4:11.

MAJIBU

A. Miaka mia moja.—Mwanzo 21:5.

B. Kupitia uzao wake mataifa yote ya dunia hakika yatajibariki.—Mwanzo 22:16-18.

C. “Rafiki ya Yehova.”—Yakobo 2:21-24.

Watu na Nchi

3. Majina yetu ni Rahela na Andrei. Sote tuna umri wa miaka saba, na tunaishi Rumania. Kuna Mashahidi wangapi wa Yehova nchini Rumania? Ni 38,600, 68,300, au 83,600?

4. Ni alama gani inayoonyesha eneo ninaloishi? Chora duara kuzunguka alama hiyo, na uchore alama nyingine kuonyesha eneo unaloishi kisha uone kwenu ni umbali gani kutoka Rumania.

A

B

C

D

Watoto Watafute Picha

Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.

● Majibu ya “MAZUNGUMZO YA FAMILIA” kwenye ukurasa wa 11

MAJIBU YA UKURASA WA 30 NA 31

1. A ng’ombe.

2. A kondoo.

3. 38,600.

4. C.