Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kadiri Wanavyokua

Kadiri Wanavyokua

Kadiri Wanavyokua

“Sisi sote tulifurahia kusoma Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia tulipokuwa watoto. Sasa tuna mwana anayeitwa Joshua mwenye umri wa miezi 16. Kitabu hicho ni kifaa kizuri cha kumfundishia. Hata akiwa na umri huo mchanga, Joshua anaweza kuwatambua watu 35 wa Biblia kwa jina katika kitabu hicho. Yeye hutumia majina yao anapozungumza.”—Timothy na Ann.

“Mwana wangu mchanga hufurahia kupitia kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu, na tayari anajua picha nyingi zilizomo. Kimenisaidia kuzungumzia pamoja naye jinsi anavyoweza kukabiliana na matatizo akiwa shuleni na kwingineko. Kitabu hicho kinafaa sana!”—Jennifer.

“Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2, kinashughulikia kila sehemu ya maisha ya vijana. Nina umri wa miaka 19. Kitabu hicho kimenisaidia kujiwekea miradi, kufanya maamuzi yenye hekima kuhusu kuanzisha urafiki wa kimapenzi, na kufanya maendeleo ili niwe na uhusiano mzuri na Mungu. Wote, vijana kwa wazee, wanapaswa kusoma kitabu hicho.”—Courtney.

Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia

Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu

Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2

□ Bila masharti, ningependa kupokea nakala ya kitabu nilichotia alama. Unaweza kutuma ombi lako kwa kujaza sehemu hii kupitia anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Ningependa kujifunza Biblia bila malipo.