Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Babu Yake Alikuwa Amekufa

Babu Yake Alikuwa Amekufa

Babu Yake Alikuwa Amekufa

● “Mimi si Shahidi wa Yehova,” ndivyo mwanamume mmoja alivyoandikia ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova huko Mexico, “lakini magazeti yenu yanapendeza sana. Moja lilitaja kuhusu broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. Hilo lilinivutia kwa sababu babu yangu alikuwa amekufa muda fulani kabla ya hapo. Ningependa kupata nakala nane za broshua hiyo niwagawie watu wa familia yangu ili niwafariji.”

Broshua Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa ina majibu ya maswali kama vile: Naweza kuishije nikiwa na huzuni yangu? Na kuna tumaini gani kwa wale ambao wamekufa? Inaonyesha kile ambacho Biblia inasema kuhusu kifo na hali ya wafu. Pia inataja kuhusu ahadi ya Mungu, kupitia Yesu Kristo, ya kuwafufua watu kwenye dunia iliyosafishwa na kufanywa kuwa paradiso.

Unaweza kuomba broshua hiyo kwa kujaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma kwa kutumia anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Bila masharti, ningependa kupokea broshua iliyoonyeshwa hapa.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.