Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Ninaweza Kupata Wapi Burudani Inayofaa?

Ninaweza Kupata Wapi Burudani Inayofaa?

Vijana Huuliza

Ninaweza Kupata Wapi Burudani Inayofaa?

Ikiwa wewe ni Mkristo, lazima uchague burudani kwa uangalifu. Hupaswi tu kutazama, kusoma, au kusikiliza kile ambacho watu wengine wanapendekeza. Kwa nini? Kwa sababu burudani nyingi siku hizi hutukuza ngono haramu, jeuri, na kuwasiliana na pepo—mambo unayopaswa kuepuka. Hata hivyo, kuna burudani inayofaa. Acha tuchunguze jinsi unavyoweza kuipata. *

SINEMA

Weka alama ya ✔ kando ya aina ya sinema unayopenda kutazama.

○ Vichekesho

○ Drama

○ Matukio yenye kusisimua

○ Hadithi za kubuniwa za sayansi

○ Nyingine

Je, wajua . . . ? India hutokeza zaidi ya sinema elfu moja kila mwaka—nyingi zaidi kuliko nchi nyingine yoyote.

Mambo ya kuepuka. Sinema nyingi huwachochea watu kufuata mambo yanayopingana na viwango vya Biblia. Baadhi ya sinema hizo huonyesha ngono na jeuri waziwazi, na nyingine pia huonyesha mambo ya kuwasiliana na pepo. Lakini Biblia inasema hivi: “Yaondoleeni mbali mambo haya yote kutoka kwenu, ghadhabu, hasira, ubaya, matukano, na maneno machafu.” (Wakolosai 3:8) Zaidi ya hilo, Mungu anashutumu matendo yoyote yanayohusiana na kuwasiliana na pepo.—Kumbukumbu la Torati 18:10-13.

Jinsi unavyoweza kuchagua. “Ikiwa sehemu fupi za sinema zinazotumiwa kutangaza sinema fulani zinaonyesha mambo yasiyofaa, basi mimi huamua sitaitazama sinema hiyo.”—Jerrine. *

“Kwa kawaida mimi sifuati mapendekezo ya mtu yeyote isipokuwa tu niwe na hakika kwamba ana viwango sawa na vyangu.”—Caitlyn.

“Ikiwa ninatazama sinema kwenye jumba la sinema halafu nianze kusumbuliwa na dhamiri, mimi huondoka mara moja.”—Marina.

“Ili nijue zaidi kuhusu sinema ninayotaka kutazama, mimi hutumia tovuti ya Intaneti inayoonyesha ikiwa sinema hiyo ina mambo ya ngono, jeuri, na lugha chafu.”—Natasha.

Dokezo: Tafuta sinema ambazo huenda zisiwe na habari isiyofaa. “Mimi hufurahia sana kutazama sinema zinazoonyesha mambo ya zamani,” anasema kijana anayeitwa Masami.

Jiulize hivi,

‘Je, sinema ninazotazama zinafanya iwe rahisiau vigumukwangu kutii amri za Mungu kuhusu ngono, jeuri, na kuwasiliana na pepo?’

VITABU

Weka alama ya ✔ kando ya habari unayopenda zaidi kusoma.

○ Hadithi za kubuniwa

○ Hadithi halisi

○ Hadithi za zamani

○ Nyingine

Je, wajua . . . ? Zaidi ya vitabu elfu moja huchapishwa kila juma nchini Marekani pekee.

Mambo ya kuepuka. Kama tu ilivyo na sinema, vitabu vingi huzungumzia viwango ambavyo Biblia inapinga. Kwa mfano, baadhi ya vitabu huwa na mambo ya ngono au ya kuwasiliana na pepo. Lakini Biblia inasema hivi: “Uasherati na ukosefu wa usafi wa kila namna au pupa visitajwe hata kidogo katikati yenu.” (Waefeso 5:3) Pia inasema kwamba matendo ya kuwasiliana na pepo ni “mabaya machoni pa Yehova.”—2 Wafalme 17:17.

Jinsi unavyoweza kuchagua. “Ninapotafuta kitabu kinachofaa, mimi husoma jalada la nyuma na pia mimi hupekua kila sura. Ninapoona habari ya kutiliwa shaka, sikinunui.”—Marie.

“Kadiri nilivyokuwa mkubwa na kuanza kujifanyia maamuzi, nilitambua umuhimu wa kuisikiliza dhamiri yangu. Nilipohisi kwamba kitabu fulani hakifai, niliacha kukisoma mara moja. Nilitambua kuwa kinapingana na maoni ya Mungu.”—Corinne.

Dokezo: Panua mapendezi yako. “Niligundua kwamba ninafurahia zaidi kusoma vitabu vya hadithi za kale kuliko vile vilivyo na hadithi za kisasa zilizobuniwa,” anasema Lara, mwenye umri wa miaka 17. “Vitabu hivyo vinavutia sana unaposoma maneno yaliyotumiwa, jinsi wahusika wanavyofafanuliwa, na jinsi hadithi yenyewe inavyotiririka!”

Jiulize hivi,

‘Je, vitabu ninavyosoma vinanitumbuiza na mambo ambayo Mungu anashutumu?’

MUZIKI

Weka alama ya ✔ kando ya aina ya muziki upendao zaidi.

○ Roki

○ Muziki wa zamani

○ Jazi

○ R&B

○ Rapu

○ Nyingine

Je, wajua . . . ? Kampuni nne kubwa za kurekodi hutoa jumla ya vibao 30,000 hivi kila mwaka.

Mambo ya kuepuka. Kama tu ilivyo na sinema na vitabu, aina nyingi za muziki wa leo huwa na mambo machafu. Maneno machafu na video za muziki zenye picha chafu zinaweza kufanya iwe vigumu kudhibiti tamaa yako ya ngono. (1 Wakorintho 6:18) Leigh, mwenye umri wa miaka 21 anasema kwamba “muziki mwingi leo huwachochea watu wajiendeshe kwa njia inayopingana na viwango vya Biblia, na mdundo wake huwachochea wacheze dansi kwa njia inayoamsha hamu ya ngono.”

Jinsi unavyoweza kuchagua. “Mimi hujiuliza, ‘Ikiwa ningewaruhusu Wakristo waliokomaa wachunguze orodha yangu ya muziki, je, ningeaibika wanapoona muziki ninaosikiliza?’ Hilo hunisaidia nichague kwa hekima muziki nitakaosikiliza.”—Leanne.

Dokezo. Uwe tayari kusikiliza mitindo mbalimbali ya muziki. “Baba yangu hufurahia kusikiliza muziki ya zamani, kwa hiyo nilisikiliza muziki wa aina hiyo tangu nilipokuwa mchanga,” anasema kijana anayeitwa Roberto. “Akili yangu ilipanuka nilipojifunza kuhusu muziki wa zamani huku nikijifunza pia kupiga piano!”

Jiulize hivi,

‘Je, muziki ninaosikiliza unafanya iwe rahisiau vigumukwangu kudhibiti tamaa ya ngono?’

SOMA ZAIDI KUHUSU HABARI HII!

Ona kitabu Maswali Ambayo Vijana HuulizaMajibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2, Sura ya 31 na 32, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

Unaweza kupata makala zaidi za “Vijana Huuliza” katika Tovuti ya www.watchtower.org/ype

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 3 Amkeni! halipendekezi wala kupinga sinema yoyote, kitabu, au wimbo. Kusudi la habari hii ni kukusaidia ukuze na ufuate dhamiri inayoongozwa na viwango vya Mungu vilivyo katika Biblia. —Zaburi 119:104; Waroma 12:9.

^ fu. 13 Baadhi ya majina katika makala hii yamebadilishwa.

[Blabu katika ukurasa wa 19]

Watayarishaji wa sinema, vitabu, na muziki hawapati hasara yoyote bali wanafaidika unapopuuza dhamiri yako iliyozoezwa na Biblia na kutazama, kusoma, au kusikiliza chochote ambacho watu wanapenda.

[Sanduku/​Picha katika ukurasa wa 18]

“Vitabu na sinema nyingi hazifai kulingana na viwango vya Biblia. Lakini ninapopata hadithi ambayo haipingani na viwango hivyo, mimi hufurahia sana kuisoma.” Adrian

[Sanduku katika ukurasa wa 18]

MBONA USIWAULIZE WAZAZI WAKO?

Ni mambo gani kuhusu burudani ambayo yamebadilika tangu mlipokuwa na umri wangu? Ni mabadiliko gani ambayo wazazi wenu waliwaeleza yalitukia kati ya wakati wao walipokuwa vijana hadi wakati wenu?

[Sanduku/​Picha katika ukurasa wa 19]

“Muziki fulani unaweza kutufanya tuvutiwe na mambo ambayo tukiwa Wakristo tunapaswa kujiepusha nayo. Hatungependa kupuuza maonyo ya dhamiri yetu nzuri kwa sababu tu tunapenda mdundo fulani.” Janiece