Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Kweli Vikusanyiko Vyote vya Kirafiki Vinapendeza?

Je, Kweli Vikusanyiko Vyote vya Kirafiki Vinapendeza?

Vijana Huuliza

Je, Kweli Vikusanyiko Vyote vya Kirafiki Vinapendeza?

Hapa chini, tia alama ya ✔ kwenye jambo unalotazamia kwa hamu sana unapoalikwa kwenye kikusanyiko cha kirafiki.

○ kula

○ kucheza dansi

○ michezo

○ kuanzisha urafiki

○ kukutana na marafiki wa zamani

○ jambo lingine

VIJANA wengi hupenda kukusanyika pamoja na rafiki zao, na hilo si jambo baya. Vikusanyiko vya kirafiki vinatajwa kwa njia inayofaa katika Biblia.

Je, ulijua?

● Wana wa Ayubu walipanga karamu za kifamilia.—Ayubu 1:4.

● Yesu alihudhuria sherehe ya arusi.—Yohana 2:1-11.

● Wakristo wa karne ya kwanza walifanya tafrija katika nyumba zao.—Matendo 2:46, 47.

Ukweli ni kwamba inafurahisha sana kukusanyika pamoja na marafiki. Lakini inasikitisha kwamba wakati mwingine, vikusanyiko fulani haviburudishi.

SIMULIZI HALISI “Nilialikwa kwenye sherehe ambayo kila mtu aliruhusiwa kuhudhuria, na ilikuwa ifanywe kwenye nyumba ya mvulana mmoja ambaye wazazi wake walikuwa wamesafiri. Niliamua sitaenda, na ninafurahi kwamba nilifanya uamuzi huo! Siku iliyofuata, nilisikia kwamba watu wengi walikunywa kileo na wengine walilewa chakari. Hata wavulana watatu walizirai kwa sababu ya ulevi. Tena, kulizuka vita, na ilibidi polisi waitwe ili kuivunja sherehe hiyo.”—Janelle.

SOMO Usipuuze mambo! Iwe unapanga kikusanyiko cha kirafiki au umealikwa tu, hakikisha unajua majibu ya maswali yaliyo kwenye kurasa zifuatazo. Ukifanya hivyo, utafurahia tafrija hiyo na hutakuwa na majuto baadaye.

WALE WALIOFANIKIWA

“Rafiki yangu alipoandaa karamu, mama yake alihakikisha anafahamu kila kitu kinachoendelea. Hata nilipoenda kwenye gari kuchukua koti, alitaka kujua ninaenda wapi. Je, kufanya hivyo ni kutahadhari kupita kiasi? Pengine. Lakini sikuudhika kwa sababu ninatambua kwamba ni afadhali kuwa mwangalifu kwa kuwa majuto ni mjukuu.”—Kim.

“Nimewahi kuwa kwenye karamu nzuri, na ninafikiri zilifaulu kwa sababu kulikuwa na watu wa umri mbalimbali. Pia, wenye kupanga vikusanyiko hivyo walitayarisha mapema vitumbuizo, kwa hiyo hakuna mtu aliyeachwa afanye jambo alilotaka tu.”—Andrea.

Unaweza kupata makala zaidi za “Vijana Huuliza” katika Tovuti ya www.watchtower.org/ype

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 26, 27]

“Kuna watu ambao ni mashirika mazuri, na kuna wale wanaojifanya kuwa wazuri lakini wakati mwingine wanajiingiza katika mwenendo usiofaa. Siri ya kupanga kikusanyiko kizuri cha kirafiki ni kukagua kwa uangalifu wageni utakaoalika.”

“Nimewahi kuhudhuria vikusanyiko vilivyopangwa vizuri na pia ambako sheria zilizingatiwa ili kusitokee matatizo baadaye. Hilo lilifanya vikusanyiko hivyo visiwe na matatizo na viburudishe kwelikweli.”

[Picha]

Nicole

Andrew

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 26]

● Ni nani watakaohudhuria, na ni wangapi?

“Nafikiri unapaswa kualika watu unaowafahamu vizuri na si yeyote tu, na usiwaambie wale uliowaalika waje na rafiki mwingine.”—Renee.

“Ikiwa idadi ya walioalikwa haitadhibitiwa, inaweza kuwa vigumu kusimamia kikusanyiko cha kirafiki. Unaalika watu 20, lakini hao 20 wanaalika wengine 10, na hao 10 pia wanawaalika wengine zaidi . . . Nimeona jambo hilo likitendeka!”—Colette.

“Vikusanyiko vya kirafiki vinapokuwa vikubwa mno, ni vigumu kuvisimamia. Nafikiri ni jambo la hekima zaidi kuwa na kikundi kidogo cha watu.”—Alexis.

“Anayetembea na watu wenye hekima atakuwa na hekima, lakini anayeshirikiana na wajinga atapatwa na mabaya.”​—METHALI 13:20

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 26, 27]

● Unatarajia ni mambo gani yatakayotokea?

“Kama wewe ndiye umeandaa karamu na mambo mabaya yatendeke, sifa yako ndiyo itakayoharibika.”—Bridget.

“Ukipanga mambo kwa uangalifu, kikusanyiko cha kirafiki kinaweza kuburudisha kila mtu. Yote yanategemea hasa uwezo wako wa kuona mambo kimbele.”—Seth.

SIMULIZI HALISI “Rafiki yangu aliniambia kuwa hanialiki kwenye vikusanyiko vyake kwa sababu anajua wazazi wangu watamwuliza maswali kama vile, Ni akina nani watakaohudhuria? na Karamu hiyo itachukua muda gani? Anasema hapendi kuchunguzwa-chunguzwa kwa njia hiyo. Hiyo ni ishara mbaya inayotoa onyo la mapema! Kama hapendi kuulizwa maswali, sidhani kama ningependa kuhudhuria vikusanyiko anavyopanga!”—Ellen.

“Kama mnakula au mnakunywa au mnafanya jambo lingine lolote, fanyeni mambo yote kwa utukufu wa Mungu.”—1 WAKORINTHO 10:31

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 26, 27]

● Utafanya nini endapo kikusanyiko cha kirafiki kinafanya usumbuliwe na dhamiri?

“Nina mpango wa kuponyokea. Ninapoenda kwenye kikusanyiko, daima mimi huwapigia simu wazazi wangu na kuwajulisha saa nitakaporudi nyumbani. Ninapofanya hivyo, wao huniuliza kama kila kitu ni shwari. Nikisema la, mara moja wananiambia kwa werevu kwamba nahitaji kurudi nyumbani ili nimalize kazi fulani za nyumbani. Nikikata simu, ninawaambia rafiki zangu kwamba wazazi wangu wananihitaji nyumbani haraka na ni lazima niondoke.”—Therese.

SIMULIZI HALISI “Kwenye kikusanyiko kimoja, wavulana wawili ambao hawakualikwa walifika, na mmoja wao alijulikana kuwa anatumia dawa za kulevya. Haikuwa rahisi kwangu kufanya uamuzi, lakini nilimpigia baba yangu simu aje kunichukua.”—Mary.

“Watu werevu huona hatari kimbele na kuiepuka, lakini asiyefikiria ataendelea mbele na kujilaumu baadaye.”—METHALI 22:3, TODAY’S ENGLISH VERSION

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 27]

● Ni nani atakayesimamia mambo?

“Ikiwa watu wakomavu watakuwepo ili kuhakikisha kila kitu ni shwari, kuna uwezekano kikusanyiko kitafaulu.”—Mark.

“Niliona aibu kuwa pamoja na wazazi wangu kwenye vikusanyiko. Lakini sasa natambua kwamba kuwapo kwao husaidia kudhibiti mambo. Haimaanishi kwamba utakosa starehe kwa sababu uko na wazazi wako kwenye kikusanyiko.”—Laura.

“Iweni na dhamiri njema.”—1 PETRO 3:16

[Sanduku katika ukurasa wa 27]

MBONA USIWAULIZE WAZAZI WAKO?

Waulize wazazi wako walifurahia vikusanyiko vya aina gani walipokuwa na umri kama wako. Je, kuna jambo lolote ambalo wangefanya kwa njia tofauti kuhusu vikusanyiko vya kirafiki ambavyo walipanga au kualikwa?

JE, UNAPANGA TAFRIJA?

Zungumza na wazazi wako na ufikirie kwa makini kuhusu . . .

1. Ni nani atakayealikwa

2. Utaalika watu wangapi

3. Tafrija itafanyiwa wapi

4. Itasimamiwaje

5. Mmepanga kuwe na utendaji gani

[Mchoro katika ukurasa wa 25]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

UMEALIKWA!