Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

‘Ujumbe Mzito Lakini Rahisi Kueleweka’

‘Ujumbe Mzito Lakini Rahisi Kueleweka’

‘Ujumbe Mzito Lakini Rahisi Kueleweka’

● Hivyo ndivyo msomaji mmoja huko Nebraska, Marekani alivyosifu kitabu alichokuwa amesoma karibuni. Aliandika hivi: “Mimi ni mwanamume mseja mwenye umri wa miaka 56 na nimemaliza tu kusoma kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Mara moja nilishangazwa sana na jinsi maneno yalivyotumiwa kwa ustadi kufafanua ujumbe mzito kwa njia rahisi sana na kwa upendo.” Aliongezea: “Picha zake ni maridadi sana. Ningekuwa baba au babu, ningewasaidia watoto wangu wadogo watumie wakati wao mwingi kuchunguza picha hizo kama ule ambao wangetumia kusoma kitabu chenyewe.”

Mwanamke mmoja huko Georgia, Marekani aliandika hivi kuhusu kitabu hichohicho: “Mpwa wangu wa kike mwenye umri wa miaka sita anayeitwa Avery, alienda nacho shuleni ili akisome pamoja na watoto wenzake wa darasa la kwanza. Baada ya kusomea wanadarasa wenzake hadithi moja, mwalimu wake alivutiwa sana hivi kwamba akafanya mpango ili Avery awe akisoma hadithi moja kutoka kwenye kitabu hicho kila siku.” Mamake mdogo aliongezea kusema: “Avery amewatolea wanadarasa wenzake na mwalimu wake ushahidi mzuri kama nini!”

Unaweza kuomba nakala ya kitabu hicho chenye kurasa 256, chenye picha maridadi, ambacho kina kurasa kubwa sawa na gazeti hili. Jaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na uitume kwenye anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Bila masharti, ningependa kupokea kitabu kilichoonyeshwa hapa.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.

[Picha katika ukurasa wa 32]

Kwa nini Msamaria alikuwa jirani mwema?