Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Sababu Iliyonifanya Niache Kazi Yenye Pesa Nyingi (Juni 2010) Sijui niwashukuru kwa njia gani kwa ajili ya makala hiyo! Nina umri wa miaka 39 na ninalea watoto watatu nikiwa peke yangu. Katika eneo la Urusi ninaloishi, si rahisi kupata ajira. Lakini mfano wa Martha Teresa Márquez ulinichochea kuchukua hatua. Makala hiyo ilisema kwamba ili ajitegemeze kifedha huku akiendelea na utumishi wa wakati wote, Martha alipika sambusa za aina fulani na kuziuza barabarani. Kwa hiyo, niliamua kuiga mfano wake na kupika vitumbua vya Kirusi vinavyoitwa piroshki. Nimefaulu! Sasa, imekuwa biashara ya familia yetu. Kwa sababu hiyo, watoto wangu wanajifunza stadi mbalimbali wanazoweza kutumia maishani na wanawajibika zaidi.

G. M., Urusi

Jinsi ya Kukabiliana na Kigugumizi (Mei 2010) Asanteni kwa kutoa habari sahihi kuhusu kigugumizi. Tunajitahidi kuwajulisha watu wenye kigugumizi kwamba kuna njia nyingi za kupata msaada wa kushinda tatizo hilo.

J. F., msimamizi wa Shirika la Kuzuia na Kutibu Kigugumizi, Marekani

Vijana Huuliza . .  . Ninaweza Kueleza kwa Njia Gani Maoni ya Biblia Kuhusu Ngono Kati ya Watu wa Jinsia Moja? (Desemba 2010) Nimekuwa katika ndoa kwa miaka kumi, na sasa nina mtoto mmoja. Ninang’ang’ana kila siku na “mwiba katika mwili” wangu. Nina tamaa ya kufanya ngono na mtu wa jinsia yangu. Kuoa hakukuondoa tamaa hiyo. Nilikuwa nimekata tamaa kwa sababu ilionekana kana kwamba nimeshindwa kupigana na tamaa hiyo. Hata hivyo, baada ya kusoma makala hiyo, sijihisi tena kama mtu asiyeweza kushinda tatizo hilo. Nimefaulu kufikia mradi wa kutotenda kupatana na tamaa hizo.​—2 Wakorintho 12:7.

Jina limebanwa, Marekani

Nimepambana na tamaa ya kufanya ngono na watu wa jinsia yangu tangu nikiwa na umri wa miaka mitano. Sasa nina umri wa miaka 61, na tamaa hizo hazijapungua. Nilipendezwa sana hasa na maelezo yaliyosema kwamba hata watu wanaovutiwa kingono na watu wa jinsia zote mbili lazima waukimbie uasherati na kwamba kuna wale “ambao hawana matumaini ya kufunga ndoa na pia wale ambao wamefunga ndoa na mtu asiyeweza kufanya ngono kwa sababu ya ulemavu fulani,” na bado watu hao huishi kwa furaha bila kutosheleza tamaa zao za ngono. Kwa hiyo, watu wenye tamaa ya kufanya ngono na watu wa jinsia yao wanaweza pia kuishi maisha safi kiadili kama kwa kweli wanataka kumpendeza Mungu. Kwa hiyo, nawashukuru kwa kututia moyo watu kama sisi tunaopambana na hali hii.

Jina limebanwa, Marekani