Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kwa Nini Nilisema Jambo Hilo?

Kwa Nini Nilisema Jambo Hilo?

Vijana Huuliza

Kwa Nini Nilisema Jambo Hilo?

Makala hii itakusaidia kuchunguza

KWA NINI mara kwa mara ulimi wako huteleza

Utafanya NINI ukiteleza

JINSI ya kudhibiti ulimi wako

“Mimi hujitahidi sana kudhibiti ulimi wangu, lakini wakati mwingine ninateleza, na ninaaibika sana!”​—Chase

“Wakati mwingine ninasema jambo ambalo huenda kila mtu anafikiria kulihusu lakini halikupaswa kusemwa hadharani.”​—Allie

KWA NINI JAMBO HILO HUTUKIA

Andiko la msingi: “Kama mtu hakosi katika usemi wake, basi, huyo ni mkamilifu.” (Yakobo 3:2, Biblia Habari Njema) Jambo kuu ni nini? Hakuna anayeweza kuongoza kikamili ulimi wake. Wengi watakubaliana na Annette, * anayekiri wazi hivi: “Nyakati nyingine mimi hujaribu kudhibiti maneno yangu lakini ninajikuta nimeongea bila kufikiri.”

Simulizi halisi: “Rafiki yangu alivutiwa na nguo nilizokuwa nikitupa. Bila kufikiria, nikasema, ‘Sidhani kama zitakutosha.’ Alijibu, ‘Ati nini? Kwani unafikiri mimi ni mnene kupita kiasi?’”​—Corrine.

Ili uelewe kwa nini huenda ulimi wako ukateleza mara kwa mara, jaribu mambo yafuatayo.

● Tambua udhaifu wako.

․․․․․ Kwa kawaida mimi huongea ninapokasirika

․․․․․ Kwa kawaida mimi huongea bila kufikiri

․․․․․ Kwa kawaida mimi husema bila kusikiliza wengine

․․․․․ Jambo lingine ․․․․․

Mfano: “Tatizo langu ni kwamba nina mzaha kupita kiasi, na wakati mwingine ninapoongea, watu hunielewa vibaya.”​—Alexis.

● Tambua ni nani ambaye ukiongea naye ni rahisi kuteleza ulimi.

․․․․․ Mzazi

․․․․․ Ndugu yako

․․․․․_ Rafiki

․․․․․ Mwingine

Mfano: “Inasikitisha, lakini watu ninaowapenda sana mara nyingi ndio rahisi kuwaumiza,” anasema Christine, msichana mwenye umri wa miaka 20. “Nadhani ni kwa sababu ninahisi nikiwa nimestarehe ninapokuwa nao ndiposa ninaacha kuwa mwangalifu.”

UTAFANYA NINI UKITELEZA

Andiko la msingi: ‘Fuatilia mambo yanayofanya kuwe na amani.’ (Waroma 14:19) Njia moja ya kufuata shauri hilo ni kuomba msamaha.

Simulizi halisi: “Mama yangu alikufa nilipokuwa na umri wa miezi kumi na baba yangu hakujishughulisha na mimi, kwa hiyo nililelewa na mamangu mkubwa na mume wake. Siku moja nilipokuwa na umri wa miaka 10 au 11, nilijihisi mpweke sana na kukasirika kwa kuwa mama yangu alikufa, na nilihisi kwamba nilitaka kumlaumu mtu fulani. Kwa hiyo mamangu mkubwa aliponiambia nimsaidie kazi fulani, nilianza kuongea kwa ukali; na mwishowe, nikaropoka na kusema ‘Sikupendi’ na ‘Wewe hata si mamangu halisi.’ Mamangu mkubwa aliniangalia kwa mshtuko. Kisha, akaingia chumbani mwake na kufunga mlango, na nilimsikia akilia. Nilijihisi vibaya sana. Alikuwa amenitunza na kunifanyia kila jambo, na sasa nilimtendea vibaya. Mume wake aliongea nami kuhusu jambo hilo na akanionyesha maandiko yanayohusu kuudhibiti ulimi. Baadaye, nilimwomba mama mkubwa msamaha. Nilihitaji kutambua kwamba nilikuwa nimekosea.”​—Karen.

Hapa chini, andika sababu zinazoweza kufanya iwe vigumu kwako kuomba msamaha.

․․․․․

Kwa nini kuomba msamaha kunaweza kufanya uhisi vizuri?

․․․․․

Dokezo: Fikiria kanuni zilizo kwenye Methali 11:2 na Mathayo 5:23, 24.

Ukweli ni kwamba ni vizuri kuzuia hali mbaya isitokee ili usihitaji kuomba msamaha. Unawezaje kufanya hivyo?

JINSI YA KUDHIBITI ULIMI WAKO

Andiko la msingi: “Uwe mwepesi kuhusu kusikia, si mwepesi wa kusema, si mwepesi wa ghadhabu.” (Yakobo 1:19) Hapa chini kuna madokezo yatakayokusaidia kutumia shauri hilo maishani

Soma maandiko yafuatayo, na upatanishe kila andiko na dokezo lake.

Methali 12:16

Methali 17:14

Methali 26:20

Mhubiri 7:9

Wafilipi 2:3

1 “Usijifikirie kupita kiasi; kwa njia hiyo hutakasirika ovyoovyo.”—Danette.

2 “Mimi huenda kutembea. Hilo hunipa fursa ya kuwa peke yangu kwa muda fulani na kuniwezesha kupunguza hasira.”—Brielle.

3 “Nilipokuwa mdogo, nilidhani ilikuwa lazima kubishania kila jambo, na nilibishania kila kitu. Lakini nimejifunza kwamba ni afadhali kuachilia mambo mengine.”—Celia.

4 “Mtu anapokufokea na umnyamazie, atachoka na kukuacha. Uwe na subira. Usiongeze kuni kwenye moto.”—Kerrin.

5 “Kuna wakati mimi humkasirikia mtu. Ninaanza kufikiria maneno ambayo ningependa kumrushia. Lakini ninapokuwa na subira, ninagundua kwamba kama ningeongea, maneno yangu hayangesaidia chochote. Nimejifunza jambo hili: usichukue hatua upesi.—Charles.

Unaweza kupata makala zaidi za “Vijana Huuliza” katika Tovuti ya www.watchtower.org/ype

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 10 Baadhi ya majina katika makala hii yamebadilishwa.

[Sanduku/Picha​katika ukurasa wa 22]

Allie​—Kabla sijasema jambo lolote, mimi hujiuliza maswali kama vile: ‘Je, hili litasaidia hali iwe nzuri? Maneno yangu yatamwathirije ninayezungumza naye?’ Ikiwa una shaka kuhusu jambo unalotaka kusema, ni afadhali kunyamaza.

Chase​—Ninapotaka kusema jambo fulani, kwanza ninajiuliza litawaathirije wale walio karibu nami. Ninafikiri kadiri ninavyozidi kuwa mtu mzima, ninapata uwezo zaidi wa kudhibiti ulimi wangu. Bila shaka unajifunza kutokana na uzoefu.

[Sanduku katika ukurasa wa 23]

MBONA USIWAULIZE WAZAZI WAKO?

Kwa kuwa sote si wakamilifu​—kama Yakobo alivyoandika, “sisi sote hujikwaa mara nyingi”—​waambie wazazi wako wakueleze wamekabili matatizo gani wanapojitahidi kuudhibiti ulimi.​—Yakobo 3:2.

[Picha katika ukurasa wa 22]

“Ukishafinya dawa ya meno kutoka kwenye tyubu, huwezi kuirudisha. Ndivyo ilivyo na usemi wetu. Tukisema jambo linaloumiza, hatuwezi kulirudisha tena mdomoni.”​—James.