Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wanathamini Upendo wa Mungu

Wanathamini Upendo wa Mungu

Wanathamini Upendo wa Mungu

● Yesu alitufundisha kuthamini upendo wa Mungu. Alisema hivi: “Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa-pekee, ili kila mtu anayemwamini asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.” (Yohana 3:16) Upendo wa Mungu kwetu na lile tumaini lenye kusisimua tulilo nalo kwa sababu ya zawadi ya Mwana wake linakaziwa katika kitabu Mkaribie Yehova.

Mwanamke mmoja huko Florida, Marekani aliandika hivi: “Baada ya kusoma sura ya 5, nilistaajabishwa na upendo, hekima, na nguvu nyingi za Yehova. Kadiri nilivyotafakari kuhusu uumbaji wake, ndivyo moyo wangu ulivyofurikwa na upendo mwingi zaidi kumwelekea.” Mwanamke fulani huko South Dakota, Marekani, alieleza hivi: “Kwa zaidi ya miaka 30, imekuwa vigumu sana kwangu kuwaonyesha wengine upendo (au kuhisi kwamba ninapendwa). Kitabu hiki kimenisaidia kuliko kitabu kingine chochote.”

Kitabu Mkaribie Yehova chenye kurasa 320 kinazungumzia sifa kuu za Yehova, yaani nguvu, haki, hekima, na upendo. Unaweza kuomba nakala ya kitabu hicho kwa kujaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na uitume kwenye anwani ifaayo kati ya zile zilizoonyeshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Bila masharti, ningependa kupokea nakala ya kitabu kinachoonyeshwa hapa.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.