Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

“Mambo ya Zamani . . . Hayataingia Moyoni”

“Mambo ya Zamani . . . Hayataingia Moyoni”

“Mambo ya Zamani . . . Hayataingia Moyoni”

Muumba wetu ametabiri jambo lenye kustaajabisha, litakaloathiri wanadamu wote. Anasema:

“Tazama mimi ninaumba mbingu mpya na dunia mpya; na mambo ya zamani hayatakumbukwa akilini, wala hayataingia moyoni.”—ISAYA 65:17.

Ni ‘mambo gani hayo ya zamani ambayo hayataingia moyoni’? Muktadha unaonyesha kwamba ni mambo kama vile ukosefu wa haki, magonjwa, kuteseka, na matatizo mengine yanayowakumba wanadamu. Matatizo haya yatakoma jinsi gani? Jibu la swali hilo linahusiana na “mbingu mpya” na “dunia mpya” zilizotabiriwa.

Maneno hayo yenye kuvutia na umuhimu wake utafafanuliwa kwenye hotuba ya watu wote yenye kichwa “Mambo ya Zamani . . . Hayataingia Moyoni.” Hotuba hiyo itatolewa kwenye Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova lenye kichwa “Linda Moyo Wako!” kuanzia mwezi wa Mei nchini Marekani na kuendelea katika sehemu nyingine duniani.

Unaalikwa kwa moyo mkunjufu uhudhurie kusanyiko litakalofanywa karibu na mahali unapoishi. Kwa habari zaidi, tafadhali wasiliana na Mashahidi wa Yehova katika eneo lenu au waandikie barua wachapishaji wa gazeti hili. Tovuti ya www.pr418.com ina orodha ya mahali ambapo makusanyiko yote yatafanywa nchini Burundi, Kenya, Kongo (Kinshasa), Malawi, Rwanda, Tanzania, na Uganda.