Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

4. Uwe Mwangalifu Unapokula Kwenye Mkahawa

4. Uwe Mwangalifu Unapokula Kwenye Mkahawa

4. Uwe Mwangalifu Unapokula Kwenye Mkahawa

Jeff, mwanamume mwenye umri wa miaka 38 aliye na afya na nguvu, aliipeleka familia yake kwenye mkahawa mmoja karibu na Pittsburgh, Pennsylvania, Marekani. Mwezi mmoja baadaye, Jeff alikufa kwa sababu ini lake liliacha kufanya kazi. Ni nini kilichosababisha hilo? Ni vitunguu vya majani alivyokula ambavyo vilikuwa na virusi vya mchochota ini aina ya A.

KATIKA nchi moja huko Ulaya, karibu nusu ya pesa zote ambazo watu hutenga kwa ajili ya chakula hutumiwa katika mikahawa. Hata hivyo, katika nchi hiyohiyo, inasemekana kwamba karibu nusu ya magonjwa yanayosababishwa na vyakula yanahusianishwa na chakula cha mikahawa.

Ni kweli kwamba unapokula kwenye mkahawa mtu mwingine ndiye anayenunua chakula na kukipika na hata kusafisha eneo la jikoni. Hata hivyo, unaweza kuamua utakula wapi, utakula nini, na ikiwa utabeba chakula kinachosalia.

Kagua mkahawa.

Daiane anayeishi Brazili anasema hivi, “Ninapoingia kwenye mkahawa kwa mara ya kwanza, mimi huangalia ikiwa meza, vitambaa vya meza, vyombo, na wahudumu ni safi na nadhifu. Ikiwa mkahawa huo si safi, sisi huondoka na kutafuta mwingine.” Katika nchi fulani, maofisa wa afya hukagua na kuipa mikahawa hiyo alama za usafi na kuandika matokeo ya ukaguzi wao kwa ajili ya umma.

Jihadhari na masalio unayobeba nyumbani.

Shirika la Usimamizi wa Chakula na Dawa la Marekani linatoa shauri hili: “Ikiwa hutafika nyumbani saa mbili baada ya kula mkahawani, usibebe masalio yoyote.” Ikiwa umebeba masalio, nenda moja kwa moja nyumbani na uyahifadhi kwenye friji hasa ikiwa halijoto ya eneo lenu inapita nyuzi 32 Selsiasi.

Ukichukua hatua nne zilizotajwa katika mfululizo wa makala hizi, unaweza kufanya chakula chako kisiwe na madhara.

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 7]

WAZOEZE WATOTO WAKO: “Sisi huwafundisha watoto wetu kuepuka kula vyakula vinavyoweza kuwadhuru.”—Noemi, Filipino