Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mazungumzo Ya Familia

Mazungumzo Ya Familia

Mazungumzo Ya Familia

Ni Nini Kimekosekana Katika Picha Hii?

Soma Mwanzo 1:21-28. Sasa tazama picha. Ni mambo gani yanayokosekana katika picha hii? Andika majibu yako kwenye mistari iliyo hapa chini. Unganisha nukta katika picha, kisha uipake rangi.

1. ․․․․․

2. ․․․․․

[Mchoro]

(Ona nakala iliyochapishwa)

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Mungu alikuwa akiongea na nani aliposema, “Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu”?

DOKEZO: Soma Yohana 17:1, 5; Wakolosai 1:15, 16.

Ni kwa njia gani wanadamu wameumbwa kwa mfano wa Mungu?

DOKEZO: Soma Wakolosai 3:10; 1 Petro 1:16.

Ni sifa gani za Yehova Mungu na Yesu zinazokuvutia zaidi? Unaweza kuiga sifa zao jinsi gani?

DOKEZO: Soma Waefeso 4:31,32; 1 Yohana 4:7, 8.

UTENDAJI WA FAMILIA:

Orodhesha wanyama watano unaowapenda zaidi. Kisha, kama Adamu, wape wanyama hao majina mapya kwa kutegemea jinsi wanavyoonekana, sauti wanayotoa, au wanavyotenda. Soma jina hilo kwa sauti na uone ikiwa wengine katika familia watajua huyo ni mnyama yupi.

Kusanya na Ujifunze

Kata, kunja katikati na uhifadhi

KADI YA BIBLIA 19 PAULO

MASWALI

A. Paulo alijitegemeza katika huduma yake kwa kutengeneza ․․․․․.

B. Mtume Paulo aliwafundisha watu “hadharani na . . .”

C. Paulo alimfufua mwanamume kijana aliyeitwa ․․․․․.

[Chati]

4026 K.W.K. Adamu aumbwa

1 W.K.

Aliishi katika karne ya kwanza W.K.

98 W.K Kitabu cha mwisho cha Biblia kinaandikwa

[Ramami]

Alizaliwa Tarso. Alitumika akiwa mmishonari huko Ulaya na Asia Ndogo

ULAYA

Roma

ASIA NDOGO

Tarso

Yerusalemu

PAULO

MAELEZO MACHACHE KUMHUSU

Zamani aliwatesa Wakristo na baadaye akageuzwa imani na kisha akawa mtume kwa mataifa. Yehova alimtumia kuandika vitabu 14 vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Paulo alisafiri maelfu ya kilomita akiwa mmishonari na kuanzisha makutaniko huko Ulaya na Asia Ndogo. —Waroma 11:13; 1 Timotheo 1:12-16.

MAJIBU

A. mahema.—Matendo 18:3-5.

B. “. . . nyumba kwa nyumba.” —Matendo 20:20.

C. Eutiko.—Matendo 20:7-12.

Watu na Nchi

3. Majina yetu ni Maté na Nia, nina umri wa miaka 7, na Nia ana umri wa miaka 8. Tunaishi katika Jamhuri ya Georgia. Kuna Mashahidi wa Yehova wangapi katika Jamhuri ya Georgia? Je, ni 10,000, 17,000, au 26,000?

4. Ni alama gani inayoonyesha eneo tunamoishi? Chora duara kuizunguka na utie alama kuonyesha eneo unaloishi kisha uone kwenu ni umbali gani kutoka Jamhuri ya Georgia.

A

B

C

D

Watoto Watafute Picha

Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.

Ili uchapishe nakala za ziada za “Mazungumzo ya Familia,” nenda kwenye www.pr418.com

● Majibu ya “MAZUNGUMZO YA FAMILIA” kwenye ukurasa wa 26

MAJIBU YA UKURASA WA 30 NA 31

1. Kiumbe kinachoruka chenye mabawa.

2. Mnyama-mwitu.

3. 17,000.

4. B.