Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Ni Nini Kitakachobadilika?

Ni Nini Kitakachobadilika?

Ni Nini Kitakachobadilika?

“Taifa halitainua upanga juu ya taifa.”

“Hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’”

“Kifo hakitakuwapo tena.”

HUENDA mambo yaliyotajwa hapo juu yakasikika kuwa ndoto tu. Lakini tunaweza kuwa na uhakika kwamba yatatimia. Kwa nini? Kwa sababu hizo si ahadi tu za wanasiasa ambao hawana uwezo wa kuubadili ulimwengu. Badala yake, ahadi hizo zinapatikana katika Biblia. *

Watu wengi wanaona kuwa Biblia ni kitabu cha kale ambacho hakina umaana wowote katika siku zetu. Je, unaamini hivyo? Ikiwa ndivyo, mbona usichunguze kwa makini yale yaliyomo katika Biblia? Kwa kweli, kati ya vitabu vyote vitakatifu, ni Biblia peke yake inayotueleza historia ya wanadamu tangu mwanzo. Inaeleza mambo yafuatayo:

● Jinsi ambavyo jamii ya wanadamu iliingia katika taabu.—Waroma 5:12.

● Jinsi Mungu anavyokusudia kurekebisha hali hiyo.—Yohana 3:16.

● Kwa nini serikali haziwezi kuubadili ulimwengu wetu.—Yeremia 10:23.

● Kwa nini tunaweza kutumaini ahadi ya Mungu kwamba atafanya hivyo.—Yoshua 23:14.

Je, kweli Mungu atawaondolea wanadamu njaa, vita, magonjwa, na kifo? Si vigumu kuamini jambo hilo ukikubali mambo yafuatayo:

1. Mungu alituumba.

2. Yeye anatujali.

3. Ana uwezo wa kuubadili ulimwengu.

4. Anakusudia kufanya hivyo.

Je, kuna sababu nzuri za kukubali mambo hayo manne? Mashahidi wa Yehova ambao huchapisha gazeti hili, wanakualika upate jibu kwa kujifunza Biblia.

Labda una Biblia lakini huisomi kwa ukawaida au hata huisomi kabisa. Hata watu wengi ambao husoma Biblia wanasema kwamba ni vigumu kuielewa. Ikiwa una maoni hayo, tunakualika uwasiliane na Mashahidi wa Yehova ili wajifunze nawe Biblia bila malipo. Mamilioni ya watu ulimwenguni pote wanafaidika na mpango huo. Mafunzo hayo huendeshwaje?

Kila juma, bila malipo yoyote, Shahidi mmoja au wawili wa Yehova watakutembelea nyumbani kwako au mahali pengine panapokufaa ili wazungumze nawe kuhusu Biblia. Mafunzo hayo ya Biblia yatakusaidia kupata majibu ya maswali kama, Kwa nini tunateseka? Kwa nini serikali za wanadamu hazina uwezo wa kuubadili ulimwengu? Ufalme wa Mungu ni nini, nao utatimiza mambo gani ambayo serikali za wanadamu haziwezi kutimiza? *

Kwa habari zaidi kuhusu jinsi unavyoweza kuwa na funzo la Biblia nyumbani kwako, wasiliana na Mashahidi wa Yehova katika eneo lenu au tembelea Tovuti yetu ya www.pr418.com. Pia unaweza kuandika barua ukitumia anwani ifaayo kati ya zile zilizoorodheshwa katika ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

[Maelezo ya Chini]

^ fu. 5 Manukuu yaliyo hapo juu yanapatikana katika Isaya 2:4; Isaya 33:24; na Ufunuo 21:4.

^ fu. 18 Ona pia makala “Maoni ya Biblia: Ni Nani Anayeweza Kuubadili Ulimwengu Wetu?” kwenye ukurasa wa 26 na 27 wa gazeti hili.