Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Unapaswa Kuanza Wakati Gani Kumfundisha Mtoto Wako?

Unapaswa Kuanza Wakati Gani Kumfundisha Mtoto Wako?

Unapaswa Kuanza Wakati Gani Kumfundisha Mtoto Wako?

● Mwanamume fulani huko Summerville, South Carolina, Marekani, aliandika kwamba tangu mke wake alipokuwa na mimba ya miezi mitatu tu, angejilaza karibu na mke wake kila usiku na kusoma kitabu cha kujifunzia Biblia kiitwacho Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. “Baada ya binti yetu, Bethiah, kuzaliwa,” baba huyo alisema, “tuliendelea na ratiba hiyohiyo​—hadithi moja kila usiku, mpaka tukamaliza kusoma kitabu hicho mara tatu.”

Anaendelea kusema: “Hata kabla ya Bethiah kuanza kuongea, tayari aliweza kuwatambua watu wengi wanaotajwa katika Biblia na angeweza kuigiza masimulizi kadhaa ya Biblia yaliyo katika kitabu hicho. Pia, alikuwa amejifunza kukariri hadithi nyingi za Biblia.”

Hadithi 116 zilizo katika kitabu hicho chenye picha maridadi, chenye maandishi makubwa, zimeorodheshwa kulingana na wakati ambapo watu wanaotajwa katika Biblia waliishi, na kwa hiyo humsaidia msomaji kufahamu mfuatano wa matukio katika Biblia. Ikiwa ungependa kupokea kitabu hicho chenye kurasa 256, jaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma kwa anwani inayofaa kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.

□ Bila masharti, ningependa kupokea kitabu kilichoonyeshwa hapa. Andika lugha unayotaka.

□ Ningependa kujifunza Biblia nyumbani kwangu bila malipo.