Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Hangeweza “Kukiweka Chini”

Hangeweza “Kukiweka Chini”

● Mwanamke mmoja huko New York, Marekani, alipendezwa sana na jinsi kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu kinavyozungumzia dini kubwa ulimwenguni. Anaeleza hivi: “Nilianza kukisoma na singeweza kukiweka chini! Asanteni sana kwa kuandaa kitabu hicho kilichoandikwa kwa usawaziko na kinachoelimisha.”

Msomaji mwingine aliandika hivi: “Nilisoma kitabu hicho kuanzia mwanzo hadi mwisho. Pia nilichunguza mengi kati ya marejeo yaliyoonyeshwa, na kwa kweli yalikuwa mengi! Ningempendekezea mtu yeyote kitabu hicho nikiwa na uhakika. Bila shaka, kuna habari fulani kuhusu imani ya Mashahidi wa Yehova, lakini hiyo ni sehemu ndogo tu ya historia hiyo yenye kupendeza ya dini.”

Unaweza kuomba kitabu hicho chenye kurasa 384 kwa kujaza sehemu iliyoonyeshwa hapa chini na kuituma kwa anwani inayofaa kati ya zile zilizoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.