Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mazungumzo Ya Familia

Mazungumzo Ya Familia

Kuna Kasoro Gani Katika Picha Hii?

Soma Luka 17:11-19. Ni mambo gani matatu katika picha hii ambayo si sahihi? Andika majibu yako kwenye mistari iliyo hapa chini, na ukamilishe picha hii kwa kuipaka rangi.

ZUNGUMZENI PAMOJA:

Mkoma mmoja alifanya nini ambacho wale wengine hawakufanya?

DOKEZO: Soma Luka 17:15, 16.

Unaweza kuigaje mfano wake?

DOKEZO: Soma Wakolosai 3:15; 1 Wathesalonike 5:18.

Unapaswa kukumbuka kumshukuru nani kila siku?

DOKEZO: Soma Zaburi 107:8; Yakobo 1:17.

UTENDAJI WA FAMILIA:

Mwombe kila mmoja katika familia aandike angalau sababu moja inayomfanya amshukuru Yehova Mungu, sababu moja inayofanya awe na shukrani kwa mshiriki fulani wa familia, na sababu moja inayofanya awe na shukrani kwa rafiki wa karibu ambaye si mtu wa familia. Kisha andikeni orodha ya mambo ambayo mnaweza kufanya ili kuwaonyesha watu hao kwamba mnawathamini.

Kusanya na Ujifunze

KADI YA BIBLIA 21 MUSA

MASWALI

A. Yehova alitumia roho yake kumwongoza Musa aandike vitabu gani vya Biblia?

B. Wazazi wa Musa walikuwa wanaitwa ________ na ________. Alikuwa mtoto wa kambo wa ________ ________.

C. Kamilisha maneno haya ya Biblia: Musa “aliendelea kuwa imara kama mtu . . . ”

MAMBO MACHACHE KUMHUSU

Musa alikuwa mtu wa kwanza katika Biblia kupewa uwezo wa kufanya miujiza, na alitumika akiwa nabii wa Mungu, hakimu, mpaji-sheria, na kiongozi katika Israeli la kale. Waisraeli walimwona kuwa mtu aliyefanya mambo mengi ya ajabu.​—Kumbukumbu la Torati 34:10-12; Kutoka 4:1-9.

MAJIBU

A. Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu, Kumbukumbu la Torati, na Ayubu, na pia Zaburi ya 90 na huenda ya 91.

B. Amramu, Yokebedi, binti ya Farao.​—Kutoka 1:15–2:10; 6:20.

C. “. . . anayemwona Yeye asiyeonekana.”​—Waebrania 11:27.

Watu na Nchi

4. Jina langu ni Mampionona. Nina umri wa miaka minane, na ninaishi nchini Madagaska. Kuna Mashahidi wangapi wa Yehova nchini Madagaska? Ni 10,000, 24,000, au 62,000?

5. Ni alama gani inayoonyesha eneo ninaloishi? Chora duara kuzunguka alama hiyo, na uchore alama nyingine kuonyesha eneo unaloishi kisha uone kwenu ni umbali gani kutoka Madagaska.

Watoto Watafute Picha

Je, unaweza kupata picha hizi katika toleo hili? Kwa maneno yako mwenyewe, eleza jambo linalotendeka katika kila picha.

 

MAJIBU YA UKURASA WA 30 NA 31

  1. Kunapaswa kuwa na wakoma 10, si 11.

  2. Wakoma katika simulizi hilo walikuwa wanaume tu.

  3. Mwanamume aliyerudi ‘alianguka kifudifudi miguuni pa Yesu, akamshukuru.’

  4. 24,000.

  5. B.