Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

KUUTAZAMA ULIMWENGU

Kuimulika Familia

Kuimulika Familia

Familia zinakabili changamoto nyingi, lakini ushauri wa Biblia usiopitwa na wakati unaweza kuzisaidia familia zishinde changamoto hizo na ziimarike.

Afrika

Kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni, akina mama wanapaswa kuanza kuwanyonyesha watoto wao ndani ya saa moja baada ya kujifungua na waendelee kufanya hivyo kwa miezi sita mfulululizo. Licha ya ushauri huo, Mshauri wa Mambo ya Lishe Mashariki na Kusini mwa Afrika wa Shirika la UNICEF alisema kwamba matangazo ya kibiashara yanapotosha watu kwa kusisitiza kwamba “maziwa ya kopo ni mazuri tu kama maziwa ya mama.”

BIBLIA INASEMA NINI? “Mtu asiye na uzoefu huamini kila neno, lakini mtu mwerevu huzifikiria hatua zake.”—Methali 14:15.

Kanada

Watafiti jijini Montreal wanasema kwamba watoto ambao wazazi wao wanawawekea sheria kali lakini hawawaonyeshi upendo wana uwezekano wa kunenepa kupita kiasi kwa asilimia 30 kuliko watoto ambao wazazi wao wanawapenda na wanawapa nidhamu yenye usawaziko.

JE, WAJUA? Njia ya kulea ambayo inawanufaisha watoto ilionyeshwa kwenye Biblia karne nyingi zilizopita.—Wakolosai 3:21.

Uholanzi

Uchunguzi uliofanywa katika familia za Kiholanzi ambazo wazazi wote wawili wanafanya kazi umeonyesha kwamba wazazi wanaotenganisha majukumu yao ya kazi na ya familia wana uhusiano mzuri na watoto wao kuliko wazazi wanaoruhusu kazi iingilie majukumu yao ya familia. Kwa mfano, kuunganisha kazi na familia kwa kupiga simu zinazohusiana na mambo ya kazini wakiwa nyumbani baada ya saa za kazi kunaweza kuwafanya wazazi washindwe kuwapa uangalifu wa kutosha watoto wao.

JAMBO LA KUFIKIRIA: “Kuna wakati uliowekwa wa kila kitu.” —Mhubiri 3:1.