Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Maswali kutoka kwa wasomaji

Maswali kutoka kwa wasomaji

“Rehani” na “muhuri” ambao kila Mkristo mtiwa mafuta anapokea kutoka kwa Mungu ni nini?—2 Kor. 1:21, 22.

Zamani, pete ya muhuri ilikandamizwa kwenye udongo wa mfinyanzi au nta ili kuhalalisha hati

Rehani: Kulingana na kitabu fulani cha marejeo, neno la Kigiriki linalotafsiriwa “rehani” kwenye 2 Wakorintho 1:22 lilikuwa “neno la kisheria na la kibiashara” likimaanisha “malipo ya awali, advansi, dhamana, ambayo inalipia mapema kiasi fulani cha gharama ya ununuzi, na hivyo inalinda haki ya kisheria ya kumiliki kitu kinachonunuliwa, au kuhalalisha mkataba.” Katika kisa cha watiwa mafuta, malipo kamili, au thawabu, yanafafanuliwa katika 2 Wakorintho 5:1-5 kuwa yanahusisha kuvaa mwili wa mbinguni usioweza kuharibika. Thawabu hiyo pia inahusisha kupokea zawadi ya kutoweza kufa.—1 Kor. 15:48-54.

Kigiriki cha kisasa kinatumia neno kama hilo kurejelea pete ya uchumba. Huo ni mfano mzuri sana kwa wale ambao watakuwa sehemu ya mke wa mfano wa Kristo.—2 Kor. 11:2; Ufu. 21:2, 9.

Muhuri: Zamani, muhuri ulitumika kama sahihi inayothibitisha umiliki, uhalali, au makubaliano. Katika kisa cha watiwa mafuta, kwa njia ya mfano ‘wanatiwa muhuri,’ au alama, na roho takatifu ili wawe mali ya Mungu. (Efe. 1:13, 14) Hata hivyo, hawatiwi muhuri wa kudumu hadi wakati fulani kabla ya mtiwa mafuta kufa akiwa mwaminifu au wakati fulani kabla ya dhiki kuu kuanza.—Efe. 4:30; Ufu. 7:2-4.