Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umesoma kwa makini matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona ikiwa unaweza kujibu maswali yafuatayo:

Kuna uthibitisho gani wa Kimaandiko kwamba Mungu huhisi maumivu yetu?

Waisraeli wa kale walipokuwa watumwa nchini Misri, Mungu aliona taabu zao na alihisi maumivu yao. (Kut. 3:7; Isa. 63:9) Tumeumbwa kwa mfano wa Mungu, hivyo tuna uwezo wa kuhisi maumivu ya wengine. Mungu anajua hisia zetu hata ikiwa nyakati nyingine huenda tukahisi kwamba hatustahili kupendwa naye.​—wp18.3, uku. 8-9.

Mafundisho ya Yesu yaliwasaidiaje watu kushinda hisia za ubaguzi?

Wayahudi wengi katika siku za Yesu walikuwa na ubaguzi. Kristo alikazia umuhimu wa kuwa wanyenyekevu na alishutumu mtazamo wa kuona jamii moja kuwa bora kuliko nyingine. Aliwahimiza wafuasi wake watendeane kama ndugu.​—w18.06, uku. 9-10.

Tunajifunza nini kutokana na sababu iliyomfanya Mungu asimruhusu Musa kuingia katika Nchi ya Ahadi?

Musa alikuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Yehova. (Kum. 34:10) Mwishoni mwa ile miaka 40 nyikani, watu walinung’unika kwa mara ya pili kwamba hawakuwa na maji. Mungu alimwambia Musa azungumze na mwamba. Badala yake, Musa aliupiga mwamba huo. Huenda Yehova alimkasirikia Musa vikali kwa sababu hakufuata maagizo yake au kwa sababu Musa hakumpa Mungu utukufu kwa kufanya muujiza huo. (Hes. 20:6-12) Jambo hilo linatufundisha umuhimu wa kumtii Yehova na wa kumpa utukufu.e.​—w18.07, uku. 13-14.

Kwa nini huenda ikawa rahisi kukosea ikiwa tutawahukumu wengine kulingana na sura yao ya nje?

Kuna mambo matatu ambayo mara nyingi huathiri maoni ya watu kuwaelekea wanadamu wenzao: rangi au jamii, hali yao ya kiuchumi, au umri. Ni muhimu tujitahidi kumwiga Mungu kwa kutowabagua wengine! (Mdo. 10:34, 35).​—w18.08, uku. 8-12.

Wakristo wenye umri mkubwa wanaweza kuwasaidia wengine katika njia zipi?

Mkristo mwenye umri mkubwa ambaye mgawo wake umebadilika bado anathaminiwa na Mungu na anaweza kufanya mambo mengi ili kuwasaidia wengine. Anaweza kuwasaidia wenzi wa ndoa ambao si waamini, kuwasaidia wasiotenda, kuongoza mafunzo ya Biblia, na kupanua utumishi wake.​—w18.09, uku. 8-11.

Wakristo wana vifaa gani kwenye Sanduku lao la Vifaa vya Kufundishia?

Kuna kadi za mawasiliano na mialiko. Pia, kuna trakti nane ambazo ni rahisi kutumia na magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Vilevile kuna broshua kadhaa, vitabu viwili vya msingi tunavyotumia kujifunza Biblia na watu, na video nne, kutia ndani video Kwa Nini Ujifunze Biblia?​—w18.10, uku. 16.

Kama andiko la Methali 23:23 linavyotuhimiza, Mkristo anaweza “kununua kweli” jinsi gani?

Hatuhitaji pesa ili kununua kweli. Hata hivyo, ni lazima tutumie wakati na jitihada ili kuipata.​—w18.11, uku. 4.

Tunaweza kujifunza nini kutokana na jinsi ambavyo Hosea alishughulika na Gomeri, mke wake?

Gomeri alifanya uzinzi mara kadhaa, lakini Hosea alimsamehe na hakuvunja ndoa yao. Mwenzi Mkristo anapofanya uasherati, mwenzi wake asiye na hatia anaweza kumsamehe. Kurudia mahusiano ya kingono pamoja na mwenzi aliyefanya uzinzi kungeondoa msingi wa talaka ya Kimaandiko.​—w18.12, uku. 13.