Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Unaweza kujibu maswali yafuatayo yanayotegemea magazeti ya Mnara wa Mlinzi ya mwaka wa 2019?

Ni nini maana ya ahadi hii ya Mungu: “Hakuna silaha yoyote itakayotokezwa dhidi yako itakayofanikiwa”? (Isa. 54:17)

Tunaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu atatulinda dhidi ya “mlipuko wa waonevu.” (Isaya 25:4, 5) Maadui wetu hawatafanikiwa kamwe kutusababishia madhara yoyote ya kudumu.—w19.01, uku. 6-7.

Mungu alitendaje kwa haki aliposhughulika na Wakanaani na Waisraeli walioasi?

Mungu alileta hukumu dhidi ya wale waliojihusisha katika matendo machafu sana ya kingono au waliowatesa wanawake na watoto. Aliwabariki watu waliotii na kuwatendea wengine kwa haki.—w19.02, uku. 22-23.

Tunaweza kufanya nini mtu ambaye si Shahidi anapotoa sala?

Tunaweza kubaki kimya na wenye heshima. Hatutashiriki katika sala hiyo kwa kusema “amina” wala hatutakubali kushikana mikono pamoja na wengine. Huenda tukaamua kutoa sala ya kibinafsi kimyakimya.—w19.03, uku. 31.

Kumtendea mtoto vibaya kingono ni dhambi nzito kadiri gani?

Ni dhambi dhidi ya mtoto, kutaniko, mamlaka za serikali na Mungu. Wazee hutii sheria za nchi zinazowataka raia waripoti kwenye mamlaka za serikali mashtaka yanayohusu visa vya kuwatendea watoto vibaya kingono.—w19.05, uku. 9-10.

Unawezaje kubadili au kuboresha nguvu zinazoongoza akili yako?

Hatua za msingi ni: Sali kwa Yehova. Tafakari ukiwa la lengo la kujichunguza. Chagua rafiki zako kwa hekima.—w19.06, uku. 11.

Tunaweza kujitayarishaje sasa kwa ajili ya mateso?

Tunahitaji kuimarisha urafiki wetu pamoja na Yehova. Tumaini kikamili na tusitilie shaka kamwe kwamba anatupenda naye hatatuacha kamwe. Soma Biblia kila siku na sali kwa ukawaida. Sadiki kwamba baraka za Ufalme wa Mungu zitatimia. Kariri maandiko unayopenda na nyimbo zinazomsifu Yehova.—w19.07, uku. 2-4.

Tunawezaje kuwasaidia watu wetu wa ukoo kuokolewa?

Ni muhimu kuwaonyesha hisia-mwenzi, kutoa ushahidi kupitia mwenendo wetu mzuri, na kuwa na subira na busara.—w19.08, uku. 15-17.

Tunaburudishwa jinsi gani kama Yesu alivyoahidi kwenye Mathayo 11:28?

Tuna waangalizi Wakristo wenye upendo, marafiki bora kabisa, na kazi bora kabisa.—w19.09, uku. 23.

Mungu anaweza kutupatiaje hamu na nguvu za kutenda? (Flp. 2:13)

Tunaposoma na kutafakari neno la Mungu, anaweza kutupatia hamu ya kufanya mapenzi yake na nguvu za kutenda. Anaweza kukuza uwezo wetu wa asili kupitia roho yake.—w19.10, uku. 21.

Ni hatua gani za hekima tunazopaswa kuchukua kabla ya kufanya uamuzi mzito?

Hatua tano za kuchukua ni: Kufanya utafiti wa kina. Sali upate hekima. Chunguza nia yako. Uwe na malengo hususa. Ona mambo kihalisi.—w19.11, uku. 27-29.

Je, wazo la kutokufa kwa nafsi lilianza Shetani alipomwambia Hawa kwamba hatakufa?

Inaonekana si hivyo. Ibilisi hakumwambia Hawa kwamba akila tunda alilokatazwa na Mungu angeonekana kwamba amekufa. Hakuna mafundisho yoyote ya uwongo ya kidini yaliyoendelea kufuatwa baada ya Gharika. Inaelekea fundisho la kutokufa kwa nafsi ya mwanadamu lilianzishwa kabla ya Mungu kuvuruga lugha wakati wa ujenzi wa mnara wa Babeli.—w19.12, uku. 15.