Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umesoma kwa makini matoleo ya Mnara wa Mlinzi ya mwaka huu? Ona ikiwa unaweza kujibu maswali yafuatayo:

Tunapaswa kuwatendeaje Wakristo watiwa-mafuta?

Tunathamini imani yao; lakini ingawa hivyo, hatuwaelekezei uangalifu kupita kiasi. Tunaepuka “kuwastaajabia watu.” (Yuda 16, maelezo ya chini) Hatuwaulizi maswali ya kibinafsi kuhusu tumaini lao.—w20.01, uku. 29.

Ni nini kinachopaswa kukusadikisha kwamba Yehova anakuona?

Biblia inaonyesha kwamba Yehova alikuona hata kabla hujazaliwa. Na anasikiliza sala zako. Anajua mawazo yako na kilicho moyoni mwako, na matendo yako yanaweza kumhuzunisha au kumfurahisha Yehova. (1 Nya. 28:9; Met. 27:11) Yehova amekuvuta kwake.—w20.02, uku. 12.

Ni mifano gani inayotusaidia kujua wakati wa kuongea na wakati wa kunyamaza?

Kwa furaha, tunazungumza kumhusu Yehova. Tunazungumza ikiwa tunaona kwamba mtu fulani anafuata njia isiyo sahihi. Wazee wa kutaniko huzungumza ikiwa kuna mtu anahitaji shauri. Hatuzungumzi (au kutoa) habari kuhusu kazi yetu inayofanywa kwenye nchi zilizo chini ya marufuku. Hatufunui habari zinazopaswa kuwa siri.—w20.03, uku. 20-21.

Kuna tofauti gani kati ya nzige wanaotajwa kwenye Yoeli sura ya 2 na wale wanaotajwa kwenye Ufunuo sura ya 9?

Andiko la Yoeli 2:20-29 linasema kwamba Mungu atawafukuza mbali nzige na kwamba anaahidi kufidia uharibifu uliosababishwa na nzige hao. Kisha, Mungu anaimimina roho yake. Mambo hayo yalitimizwa wakati taifa la Israeli lilipovamiwa na Wababiloni na baada ya hapo. Andiko la Ufunuo 9:1-11 linawazungumzia watiwa-mafuta katika siku zetu ambao wanalinganishwa na nzige wanapotangaza hukumu za Mungu dhidi ya mfumo huu mwovu, na kuwafanya wale wanaouunga mkono wasiwe na amani.—w20.04, uku. 3-6.

Mfalme wa kaskazini ni nani leo?

Urusi na nchi zinazoiunga mkono. Zimewaathiri moja kwa moja watu wa Mungu kwa kupiga marufuku kazi ya kuhubiri na kuonyesha kwamba wanawachukia Mashahidi. Mfalme wa kaskazini amekuwa akipambana na mfalme wa kusini.—w20.05, uku. 13.

Je, zile sifa tisa zinazotajwa kwenye Wagalatia 5:22, 23 ni orodha kamili ya sifa za “tunda la roho”?

Hapana. Roho takatifu inatusaidia kusitawisha sifa nyingine nzuri, kama vile uadilifu. (Efe. 5:8, 9)—w20.06, uku. 17.

Mojawapo ya hatari za kuweka habari mbalimbali kujihusu mtandaoni ni ipi?

Mambo tunayoweka mtandaoni yanaweza kuwapa wengine picha ya kwamba tunajivuna, na si kwamba tuna sifa ya unyenyekevu.—w20.07, uku. 6-7.

Wahudumu wa Kikristo wanaweza kujifunza nini kutoka kwa wavuvi wenye ustadi?

Wao huvua wakati na mahali ambapo kuna uwezekano mkubwa zaidi wa kupata samaki. Wamezoezwa kutumia vifaa sahihi. Wanafanya kazi kwa ujasiri kwenye hali zinazobadilika-badilika. Tunaweza kufanya vivyo hivyo katika huduma yetu.—w20.09, uku. 5.

Ni zipi baadhi ya njia za kuwasaidia wanafunzi wetu wa Biblia waongeze upendo wao kwa Mungu?

Tunaweza kuwatia moyo wasome Biblia kila siku na kutafakari kuhusu mambo waliyosoma. Na tunaweza kuwafundisha jinsi ya kusali.—w20.11, uku. 4.

Maneno: “Katika Kristo wote watafanywa kuwa hai,” yanawahusu akina nani?—1 Kor. 15:22.

Mtume Paulo hakuwa akisema kwamba kila mwanadamu angefufuliwa. Alikuwa akiwarejelea Wakristo watiwa-mafuta, wale ambao ‘wametakaswa katika muungano na Kristo Yesu.’ (1 Kor. 1:2; 15:18)—w20.12, uku. 5-6.

Wakristo watiwa-mafuta watafanya nini baada ya ‘kubadilishwa, kufumba na kufumbua jicho, wakati wa tarumbeta ya mwisho’?—1 Kor. 15:51-53.

Watashiriki pamoja na Kristo katika kazi ya kuwachunga watu kwa fimbo ya chuma. (Ufu. 2:26, 27)—w20.12, uku. 12-13.